Habari tulizozipata hivi punde katika
chumba cha habari kutoka katika mtaa wa Mwandu kata ya
Tinde katika wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga ni kwamba mwanamme
mmoja ambaye jina lake halijajulikana mara moja amemuua mke wake kwa
kumchapa makonde kutokana na kile kinachoelezwa kuwa kwanini amechagua
mgombea wa CCM badala ya mgombea wa Chadema katika uchaguzi wa serikali
za mitaa uliofanyika nchi nzima leo.
Inaelezwa kuwa Jamaa ni mfuasi wa Chadema huku mke wake alikuwa mfuasi wa CCM.
Tukio limetokea jioni ya leo baada ya mume kumuuliza mkewe kampigia mgombea wa chama kipi leo,mke aliposema CCM ndipo mme akaanza kumpa kipigo hadi mauti kumfika.
Mdau aliyeko eneo la tukio Paul De Nyoso Seseja anasema kuna taarifa kuwa jamaa alikuwa amebugia pombe na mpaka sasa yuko kwenye mikono ya dola.
Inaelezwa kuwa Jamaa ni mfuasi wa Chadema huku mke wake alikuwa mfuasi wa CCM.
Tukio limetokea jioni ya leo baada ya mume kumuuliza mkewe kampigia mgombea wa chama kipi leo,mke aliposema CCM ndipo mme akaanza kumpa kipigo hadi mauti kumfika.
Mdau aliyeko eneo la tukio Paul De Nyoso Seseja anasema kuna taarifa kuwa jamaa alikuwa amebugia pombe na mpaka sasa yuko kwenye mikono ya dola.
إرسال تعليق