Historia ya Ukimwi na ugunduzi wa ARV - 4

Wiki iliyopita tuliona wakati ugonjwa wa Ukimwi ukiwa haufahamiki chanzo chake, wataalamu wengi wa afya walikuwa wakihangaika kufanya utafiti.
Tukaona wanasayansi wawili, Dk Paul Volberding na Dk Marcus Conant walifanikiwa kubaini uhusiano kati ya ugonjwa huo na aina ya saratani ya ngozi iliyokuwa ikiwapata wazee.
Waliweza kuihitimisha kwa kusema kuwa ugonjwa huo unatokana na virusi hasa ukizingatia kuwa dalili ya saratani hiyo iliyokuwa inawaandama wazee tu wakati huo ilihamia kwa vijana.
Saratani hiyo ya ngozi kwa wazee ikijulikana kama KS wao walichokifanya ni kuuita ugonjwa huo ambao bado ulikuwa hauna jina, KSOI.
KSOI wakiwa na maana ya ugonjwa unaowezesha mtu kufikia hatua ya kuwa na saratani ya KS.
Kwa kutamka tu kwamba ugonjwa huo unatokana na virusi mwaka 1981, wanasayansi hao walitoa mchango wao katika mikakati ya kuuchunguza zaidi.
Katika historia hiyo, leo tutajikita katika kueleza wanasayansi walioipambazua dunia kwa kuweka wazi namna virusi hao wanavyosababisha Ukimwi.
Sayansi na ugunduzi huo ndiyo uliotoa mwanya wa kutengeneza Dawa za Kufubaza virusi hao wa Ukimwi (ARV) za kuaminika miaka ya 1990.
Wagunduzi wa VVU
Mwanasayansi wa kwanza kutangaza kuwa ameweza kuviona Virusi Vya Ukimwi (VVU) ni Mtaalamu wa Kifaransa, Dk Luc Montagnier.
Mtaalamu huyo ambaye aliongoza jopo la wanasayansi wengine katika taasisi ya Pasteur ya mjini Paris alitoa ripoti yake katika jarida la sayansi mwaka 1983.
Katika utafiti huo alihusisha virusi hao na uvimbe wa kwenye mashavu unaosababishwa na mafindofindo ambayo yalikuwa yanawaandama sana wagonjwa wa Ukimwi.

Post a Comment

أحدث أقدم