![happy 12](http://i2.wp.com/sammisago.com/wp-content/uploads/2014/12/happy-121.jpg?resize=465%2C596)
Mwakilishi wa Miss World 2014 ametulita
pamoja kama nchi kwenye kumpa ushirikiano katika kupiga kura ili ashinde
peoples choice awards na kuingia kwenye top ten ya miss world. Ingawa
hatukufanikiwa kumweka namba moja Happy ameonekana mtu mwenye kujiamini
na kujituma sana. Hizi ni picha zake kwenye show ya Miss World na ujumbe
wake baada ya show kuisha.
![happy 14](http://i0.wp.com/sammisago.com/wp-content/uploads/2014/12/happy-14.jpg?resize=559%2C540)
![happy 15](http://i1.wp.com/sammisago.com/wp-content/uploads/2014/12/happy-15.jpg?resize=597%2C577)
Watanzania wenzangu na marafiki kutoka mataifa mengine, tumepiga kura sana, mmeonyesha support kubwa kuliko matarajio ya wengi bahati mbaya kura hazikutosha.
Natumia nafasi hii kuwashukuru wote mmoja mmoja kwa kuniunga mkono kwa kipindi chote ambacho nilikua hapa jijini #London na tokea niliposhinda mashindano ya #MissTanzania. Nisingefika hapa bila support yako. From deep inside my heart. I thank you.
Kuanzia aliyetumia muda na pesa yake kunipigia kura, aliyeandika na kutangaza habari yangu, designers mbalimbali, familia yangu, marafiki wote, wote, wote, I thank you.
Nimejifunza vitu vingi sana kipindi chote hiki na kwakweli watanzania tumeonyesha umoja wa hali ya juu sana. Umoja wetu na udumu katika mambo yote ya kimaendeleo kwa taifa letu.
Mbarikiwe
#Happiness4MissWorld ”
Hongera Happy kwa Ulipotufikisha.
إرسال تعليق