Wananchi wa Zanzibar wapo katika matayarisho ya kupiga kura ya
maoni ya Katiba Inayopendekezwa baada ya Bunge la Katiba kukamilisha
majukumu yake Oktoba mwaka huu na kubakia kura ya maoni mwakani.
Upingaji wa kura utatanguliwa na elimu ya uraia
ambayo itatolewa na kamati maalumu ambazo zitaundwa kwa ajili ya
kufanikisha kazi hiyo mbali na makundi ya wanaharakani na vyama vya
siasa.
Kama Katiba hiyo itafanikiwa kupita, Tanzania
itakuwa imeandika historia mpya baada ya miaka 50 kuandika Katiba
inayotokana na ushirikishwaji wa wananchi wa pande mbili za Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar.
Maneno mawili yametawala sana katika mijadala
Zanzibar hasa katika mabaraza ya kahawa na masikani watu kwa makundi ya
vijana, wazee na wanasiasa wakitumia muda mwingi kubishana kama Katiba
Inayopendekezwa itapita au.
Matokeo ya kura ya maoni yanasubiriwa kwa hamu kwa
sababu ndiyo dira ya kutoa mwelekeo wa Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa
kufanyika Oktoba mwakani.
Makundi yaibuka
Tayari kumeibuka makundi matatu Zanzibar, kila moja likiwa na mtazamo wake kuhusu kura ya maoni.
Wapo wanaofanya kampeni ya kutaka kuungwa mkono
kwa maana ya kupigiwa kura ya ndio, wengine wanaendesha kampeni ya
kutaka wananchi wapige kura ya hapana, lakini kundi la tatu linalofanya
kampeni ya kuwataka wananchi kususia zoezi zima la kura ya maoni
itakayofanyika mwakani.
Kususia kura
Waziri wa zamani wa SMZ, Mansoor Yusuph Himid
amekuwa mwanasiasa wa kwanza kujitokeza hadharani na kuwataka
Wazanzibari kususia kura ya maoni kwa madai Katiba Inayopendekezwa ni
kitanzi kipya kwa Zanzibar kiuchumi na kisiasa.
Anasema kwamba kitendo cha Wazanzibari kushiriki
kura hiyo ni sawa na mtu kushiriki kula chakula ambacho hakushiriki
kupanga bajeti, kupika au kupakua.
Mansoor, aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali
ndani ya CCM na SMZ, anakwenda mbali zaidi kwa kusema kama Katiba hiyo
itapitishwa, Zanzibar itaendelea kubanwa katika kujiamulia mambo yake ya
kiuchumi na kisiasa.
- Mwananchi
- Mwananchi
Post a Comment