Mwakalebala awezesha ligi soka ngazi ya wilaya

wenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Iringa, Cyprian Kwiyhava akimkadhi vifaa vya michezo, Shabani Magoma ambaye ni meneja wa Gangilonga FC inayoshiriki ligi ya wilaya Iringa Mjini inayodhaminiwa na Frederick Mwakalebela.


Kamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Iringa Mjini, Frederick Mwakalebela ametoa tena zaidi ya Sh Milioni 14 kudhamini ligi ya soka ngazi ya wilaya, Iringa Mjini.

Hiini mara ya pili kwa mdau huyo wa soka aliyewahi pia kuwa Katibu wa Shirikishola Soka Tanzania (TFF) kuidhamini ligi hiyo ambayo kabla yake ilikuwa ikichezwa bila washindi kupata zawadi yoyote ile.

KatibuMsaidizi wa Chama cha Soka Iringa Mjini (IMFA), Rashid Shungu alisema katika hafla fupi ya uzinduzi wa ligi hiyo mjini hapa jana kwamba: “baada ya Mwakalebela kujitokeza kudhamini ligi hii, timu zote zinapata vifaa vyamichezo, mashindi wa kwanza hadi wa tatu wanapata zawadi na waamuzi na viongoziwanaosimamia ligi hiyo wanapata posho.

Alisemakwa kupitia udhamini huo, mshindi wa kwanza anapata kikombe, Sh 500,000 namipira mitano, mshindi wa pili anapata sh 300,000 na mipira mitatu na mshinditatu anapata Sh 200,000 na mipira miwili.

Akikabidhi vifaa (jezi na mipira kwa timu hizo), Mwenyekiti wa Chama cha soka Mkoa waIringa (IRFA), Cyprian Kwihyava aliahidi kumuongezea mshindi wa kwanza wa ligihiyo, Sh 500,000 na hivyo kufanya mshindi atakayepatikana mwaka huu kuondoka najumla ya Sh Milioni moja.

Kwihyavaalisema wananchi wa mkoa wa Iringa wana kiu kubwa ya kuona moja au zaidi yatimu zake zinapata mafanikio katika mchezo huo na kushiriki ligi kuu Tanzaniabara.

Akitoasababu ya kudhamini ligi hiyo, Mwakalebela alisema: “ligi hii ni moja ya liginyingi za chini zinazoweza kusaidia kuibua vipaji vinavyoweza kuboresha mchezohuu mjini Iringa.

Alisemaakiwa mmoja wa wadau wa soka nchini, ameamua kurudi nyumbani Iringa nakushirikiana na wadau wengine kuinua mchezo huo.

“Pamojana udhamini wangu, natoa wito kwa wadau wengine wajitokeze kuziunga mkono timuzetu ili malengo tuliyonayo katika sekta hiyo yaweze kufikiwa,” alisema.

Timu zitakazoshiriki ligi hiyo ni pamoja na Gangilonga FC, Mkimbizi United, IlalaFC, Feed Force FC, Miyomboni FC, Mkwawa FC, Black Eagle FC, Iringa Downtown FC,Upendo Shooting Stars, Black Cheaters FC na Young Boys.
 Source:Picha, stori na Frank Leonard,Iringa Press

Post a Comment

Previous Post Next Post