‘Pimeni afya mjue hali zenu mapema’

Dar es Salaam. Imeelezwa kuwa vijana wengi hupoteza maisha wakiwa na umri mdogo kutokana na sababu mbalimbali, ikiwamo kutokuwa na utaratibu wa kupima afya mara kwa mara ili kubaini magonjwa kabla hayajakomaa.
Hayo yalisema jana na Katibu wa Umoja wa Vijana wa Wanakahama, Daud Ng’osha wakati wa kuhamasisha jamii kupima afya mara kwa mara.
Alisema hivi vijana wengi wamekata tamaa ya kuishi miaka 50 kutokana na kuandamwa na magonjwa ambayo yangeweza kuzuilika kama yangegundulika mapema kwa utaratibu wa kupima afya.
“Vijana wanakata tamaa kutokuwa na utamaduni wa kupima afya mara kwa mara,” alisema.
“Lengo la kuunda umoja huu ni kuikumbusha jamii kuwa na utaratibu wa kupima afya ili kujitambua na kuishi maisha ya amani, kwani sasa vijana wengi wamekata tamaa ya kuishi miaka mingi,” alisema Ng’osha.
Awali, Mwenyekiti wa Wanakahama, Sweetbert Nkuba aliwahimiza vijana na jamii kujitokeza kwa wingi kupima afya, kwani magonjwa mengi yanatibika yaligundulika mapema.
Tunapaswa kupima afya ili kubaini matatizo mapema na kuyashughulikia,” alisema Nkuba.

Post a Comment

أحدث أقدم