Tiba ya saratani kutolewa kwa njia ya mtandao

Dar es Salaam. Wagonjwa wa saratani wa mikoani wanatarajiwa kupata matibabu ya kwa njia ya mtandao baada ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kuzindua huduma ya afya ya mtandao.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja TTCL, Laibu Leonard alisema hayo juzi alipokabidhi msaada wa vyakula wa Sh3 milioni katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road.
Alisema huduma hiyo itamwezesha mgonjwa kupata matibabu akiwa katika moja ya hospitali za rufaa nchini.
Laibu alisema hata tiba ya mionzi itafanyika kwa kushirikisha madaktari bingwa waliounganishwa na huduma hiyo ya kisasa zaidi.
“Hakuna haja ya kwenda India, Uingereza, Ujerumani au nchi nyingine kwa ajili ya tiba, unaweza kufanyiwa upasuaji Bugando, Ocean Road, KCMC au Tumbi,” alisema.
Alisema lengo lao ni kuunganisha hospitali zote za rufaa nchini ifikapo Machi mwakani.
- Mwananchi

Post a Comment

أحدث أقدم