MSANII
wa filamu aliyejikita kumtumikia Bwana kwa nyimbo za Injili, Sara
Mvungi amesema kuwa, amechoshwa na upweke wa muda mrefu kwa kuishi bila
mwanaume kwa takriban miaka 10 kwa kuwa anasubiri Mungu amshushie mume
mwema.
Msanii wa filamu aliyejikita kumtumikia Bwana kwa nyimbo za Injili, Sara Mvungi.
Akitoa la rohoni kwa paparazi wetu, Sara alisema hajajihusisha na
masuala ya mapenzi kwa kuwa wanaume wengi wanaomfuata hawaamini, wengi
wao ni waongo hivyo anatamani Mungu amshushie chaguo stahiki
litakaloufariji mtima wake.
“Ni kipindi kirefu sasa, tangu mwaka 2004 naishi bila mwanaume wala kufanya starehe ya mwili na kama unavyojua suala la zinaa bila ya kuwa kwenye ndoa halimpendezi Mungu na haliendani kabisa na ulokole nilionao, natamani sana kuolewa hata leo lakini sijamuona mkweli katika wote wanaonifuata,” alisema Sara.
![](http://api.ning.com:80/files/Ktsylelmf0kqcHW8eUdKm8pA9gizjm4s86F7wi*ayfwIYePcqT59gY609Wy2oxynQiUsrPSKRXrgi8225y3kaR0v3Axaz6HQ/rasahmvungi11.jpg?width=650)
“Ni kipindi kirefu sasa, tangu mwaka 2004 naishi bila mwanaume wala kufanya starehe ya mwili na kama unavyojua suala la zinaa bila ya kuwa kwenye ndoa halimpendezi Mungu na haliendani kabisa na ulokole nilionao, natamani sana kuolewa hata leo lakini sijamuona mkweli katika wote wanaonifuata,” alisema Sara.
إرسال تعليق