
Akizungumza jana, Dar es Salaam, Mratibu wa Sekta
Binafsi yaUlinzi wa Jeshi la Polisi, Adam Maro alisema maandalizi ya
sheria hiyo yameshakamilika na kinachosubiriwa ni kupelekwa bungeni.
Alisema licha ya kuwapo kwa idadi kubwa ya kampuni
za ulinzi, nyingi zinafanya kazi bila kufuata utaratibu ikiwamo wa
kuajiri wafanyakazi wazee na kuwalipa wafanykazi wao mishahara
isiyostahili.
Akimwakilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini
(IGP), Ernest Mangu katika sherehe za Kampuni ya Ulinzi ya Security
Group Afrika (SGA) iliyotimiza miaka 30, Maro alisema sheria hiyo
itakuwa silaha ya kudhibiti kampuni zisizofuata sheria, kanuni na
utaratibu.
“Kampuni nyingi hazina vifaa vya kutosha, matokeo
yake zinashindwa kupambana na wahalifu na kusababisha hasara kwa
wateja,” alisema Maro.
Alisema kutungwa kwa sheria hiyo kutazifanya
kampuni nyingi ziungane ili ziwe na mitaji mikubwa itakayowawezesha kuwa
na vifaa vya kisasa.
“Utashangaa mtu ana mtaji Sh3 milioni anataka
kusajili kampuni ya , matokeo yake unakuta wanalinda kwa kutumia
svirungu,” alisema Maro.
Alisema Tanzania inazihitaji kampuni binafsi za
ulinzi kwa kuwa kuna upungufu wa askari polisi ambao kwa sasa kila
askari mmoja analinda watu 1,100 badala ya 450, lakini nyingi hazina
msaada hivyo kuongeza mzigo kwa Jeshi la Polisi badala ya kusaidia.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa SGA, Eric Sambu
alisema changamoto zinazoikabili kampuni hiyo ni msongamano wa magari
ambao husababisha kuchelewa kufika katika matukio.
“Barabara bado zinajengwa, nyingine zimefungwa ili
kupisha ujenzi, hiyo ni changamoto kubwa inayosababisha tushindwe
kufika kwenye matukio kwa wakati,” alisema.
إرسال تعليق