Akizungumza na vijana kutoka vyuo mbalimbali
jijini Mwanza, Makamba alisema fedha zilizochukuliwa ni za umma na
inapaswa waelewe kuwa kiongozi yeyote yupo kwa ajili ya kumsaidia
mwananchi na si kumkandamiza.
Alimshukuru Mungu akisema kuwa ‘mvua hiyo ya
manyunyu’ inawanyeshea wengine, yeye hausiki kwa lolote kuhusu fedha
hizo. “Dalili ya ngozi au manyoya ni dhahiri kuwa kuna mnyama kachinjwa
na waliohusika katika uchinjaji huo wawajibishwe kwa kufikishwa
mahakamani,” alisema Makamba.
Alisema Taifa haliwezi kujengwa kwa wizi au
udokozi na ili kusaidia Taifa ni lazima hatua madhubuti zichukuliwe au
itolewe adhabu ambayo itasaidia kukomesha wizi wa aina hii, ili na
wengine nao wajifunze.
- Mwananchi
- Mwananchi
إرسال تعليق