Utawala wa Muda wa Kusini Magharibi mwa Somalia waanza mchakato wa kujenga dola


Na Shukri Mohamed, Mogadishu

Utawala wa mpya wa Muda wa Kusini Magharibi mwa Somalia (ISWA) unatafuta suluhisho la haraka la hali iliyopo ya kukosekana kwa usalama na unafanya kazi katika kuileta jamii pamoja ambayo awali ilipinga uundwaji wake.

Rais wa Utawala wa Muda wa Kusini Magharibi Sharif Hassan Sheikh Adan akihutubia umati wa watu wakati wa mkutano uliofanyika tarehe 20 Disemba pamoja na viongozi na wazee wa ndani huko Barawe. [UN Photo/ Ilyas Ahmed]

Tarehe 17 Novemba, wajumbe kutoka mikoa ya Bay, Bakol na Shabelle ya Chini walimchagua aliyekuwa spika wa bunge la serikali ya mpito ya shirikisho Sharif Hassan Sheikh Adan kuwa rais wa dola mpya ya shirikisho kwa kipindi cha miaka minne.

Lakini kabla ya kuchaguliwa kwa Adan, jambo ambalo lilipokelewa vizuri na serikali ya shirikisho ya Somalia na wadau wa kimataifa, kulikuwa na malalamiko Baidoa, kupinga nafasi ya utawala mpya.

Wasiwasi ulikuwa unahusiana na madai ya kambi mbili za upinzani ambazo kila moja ilihamasisha uundwaji wa dola ya mikoa sita na dola ya mikoa mitatu, ambapo kila moja ilitaka kuwa na rais wake.

Baada ya mazungumzo kadhaa yaliyosimamiwa na serikali ya shirikisho, kambi ya mikoa sita, inayoongozwa na Madobe Nunow Mohamed, ilikubali kuridhia dola ya mikoa mitatu na kuingia katikamakubaliano ya kushirikiana madaraka.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, viongozi kutoka katika utawala wa mikoa sita, ambao pia unajumuisha Gedo, Jubba ya Chini na Jubba ya Kati, watahudumu nafasi ya makamu wa rais na spika wa bunge katika ISWA.

Mikoa ya Gedo, Jubba ya Chini na Jubba ya Kati tayari zilishaunda Utawala wa Muda wa Jubba, ambao una matatizo madogo yake yenyewe ulioundwa chini ya mfumo wa serikali ya shirikisho.



Wanazuoni na wazee kutoka kambi inayounga mkono utawala wa mikoa sita wanahitaji kutulizwa kisiasa, alisema Ibrahim Muse Herow, mkuu wa Chama cha Wanazuoni wa Bay na Bakol, kikundi cha wataalamu kutoka nyanja mbalimbaliu ambao wanafanya kazi kwenye masuala yanayohusiana na maridhiano na utawala.

"Uanzishaji wa utawala huo ulipingwa ," Herow aliiambia Sabahi. "Baadhi waliunga mkono mikoa sita na baadhi walitaka mikoa mitatu, na mpaka sasa hakukuwa na suluhisho kamili. Hata hivyo, inaonekana kama kwamba kambi ya Sharif Hassan imeenea na inapokea msaada wa serikali na wa jumuiya ya kimataifa."

Utawala mpya unaweza kufanikiwa kama utachukua hatua sahihi, alisema.

"Sharif Hassan inabidi ateue baraza la mawaziri ambalo lina uwiano na kuridhisha koo zote kwa kuwa kwa sasa Somalia inashirikiana madaraka kwa kuzingatia koo," Herow alisema.

"Mikoa hii pia inapata ukame unaojirudia na njaa ambayo inasababisha vifo vya mamia ya watu kila mwaka. Utawala mpya inabidi uje na mpango wa kuwaokoa watu wanaokufa," alisema.

ISWA kwa sasa inakamilisha muundo wake wa utawala, kuteua mawaziri wake na wakurugenzi wa ofisi za umma, na baadaye itaendelea katika kuunda utawala wa wilaya, alisema msemaji wa ISWA Siad Sheikh Dahir.

"Wakati uteuzi wa mawaziri na watawala wa wilaya utakapokamilika, inabidi tukabiliane na kazi muhimu sana, ambayo ni kuboresha maisha ya watu na utafutaji riziki wa msingi," aliiambia Sabahi.

Utawala utafanya kazi ya kurudisha miundombinu ya umma iliyoharibika wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe, kama vile shule, barabara na hospitali, alisema. Pia unapanga kurudisha usalama na kukomboa miji ambayo bado iko chini ya udhibiti wa al-Shabaab.

Mkaazi wa Baidoa Abukar Sidow, mwenye miaka 34, alisema alifurahi aliposikia kwamba pande mbili zinazopingana zimefikia makubaliano na sasa zinalenga kujenga upya mikoa mitatu.

"Baidoa ilikuwa katika hatari ya kuingia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe, na kulikuwa na kutoelewana kwa kiasi kikubwa katika utawala," aliiambia Sabahi. "Lakini sasa hali inaonekana kutulia, na watu wote wameelekeza macho yao kwenye utawala mpya na matumaini makubwa ya kubadili mazingira ya kisiasa na hali ya maisha katika mikoa hiyo."

Sidow aliiomba serikali ya shirikisho kuongeza mara mbili msaada wake kwa ajili ya taifa jipya ili mfumo wa shirikisho uweze kufaulu na Somalia iweze kufanya uchaguzi mwaka 2016.

Post a Comment

أحدث أقدم