Wananchi wamekata tamaa vita dhidi ya rushwa

Anasema hali hiyo si nzuri na inatoa changamoto mpya katika vita dhidi ya rushwa hasa kutokana na wananchi wengi kupoteza imani katika vita hiyo, kwa kuwa ndiyo wanaoathirika moja kwa moja na hawaoni hatua zozote madhubuti kukomesha na kuwashughulikia watuhumiwa wa matukio hayo.
“Kwa viwango hivyo vya kimataifa, Watanzania wamekuwa wakitoa mara chache chini ya wastani wa kimataifa katika masuala yanayohusiana na ardhi kwa asilimia 10 ikilinganishwa na wastani wa kimataifa wa asilimia 21 na asilimia tano katika elimu ambayo ni chini ya wastani wa kimataifa wa asilimia 16,” inaeleza ripoti hiyo.
Uthibitisho huo unadhihirisha namna ambavyo Watanzania wamekuwa wakisumbuliwa na kulazimishwa kutoa rushwa wanapopata matatizo yanayohitaji huduma ya taasisi hiyo muhimu ya usalama kwa umma ambayo inaendeshwa na Serikali kwa asilimia 100.
Mushi anasema Watanzania pia wamekuwa wakiingia katika mtego wa kutoa rushwa baada ya kutembelea ofisi za Serikali au watoa huduma katika sekta binafsi kama kamati za maji za vijiji, mashirika yasiyo ya kiserikali, mashirika ya dini au shule zilizo katika maeneo yao.
Katika mahojiano ya utafiti huo, idadi kubwa ya wananchi walisema waliwahi kuombwa rushwa na watu watatu kati ya watano, sawa na asilimia 60 waliombwa rushwa na polisi na mmoja kati ya watatu (asilimia 34) waliombwa rushwa walipokuwa wakitafuta kazi.
Katika mahojiano zaidi kuhusu mara ngapi waliwahi kuombwa rushwa, walisema polisi ndio wanaoongoza kwa kuomba rushwa na asilimia 41 walitoa kwa kuambiwa na asilimia mbili walitoa bila kuambiwa.
“Tatizo kubwa hapa ni kwamba wananchi wamepoteza imani kabisa kwa sababu hata zile kesi kubwa za rushwa zinazoibuliwa, mara nyingi zimekuwa zikipotelea hewani na hakuna anayewajibishwa,” anasema Mushi na kuongeza:
“Hata Takukuru iliyopewa jukumu la kuchunguza haijapewa meno ya kutosha.
Wananchi walisema wazi kwamba wanapenda kuiona taasisi hiyo ikiwa na uwezo wa kusimamia uchunguzi na hata kuendesha kesi hizo yenyewe, yaani iwe na uwezo wa kufuatilia mwanzo hadi kutoa uamuzi wa mwisho.”
Kwa kutumia utafiti wa kipimo cha rushwa duniani wa 2013, uliofanywa na shirika la Transparency International, Watanzania wamekuwa wakilipa hongo mara nyingi zaidi kwa maofisa wa polisi kuliko wastani wa kimataifa ambao ni asilimia 34.
Uelewa wa wananchi kuhusu rushwa kubwa
Hata hivyo, wakati rushwa ikishtadi nchini, Watanzania wengi hawana taarifa za kutosha na wengi zaidi hawajui kabisa kuhusu kashfa kubwa za rushwa zinazoelezwa katika vyombo vya habari
- Mwananchi.

Post a Comment

أحدث أقدم