Dar es Salaam. Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema pamoja na kutoa
maazimio manane kuhusu uchotwaji wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya
Tegeta Escrow, Bunge limefanya makosa ya kutozijumuisha Wizara ya Fedha
na ile ya Viwanda na Biashara katika uchunguzi huo kwa kuwa nazo
zinahusika.
Akizungumza katika mahojiano maalumu ofisini kwake
Dar es Salaam jana, Jaji Warioba alitaja mambo manne aliyoyatilia shaka
katika uamuzi huo wa Bunge, akisema yalilenga kulindana.
Mambo hayo ni msingi wa hukumu kwa watuhumiwa,
wahusika wengine kutotajwa, mwingiliano wa mamlaka ya mihimili ya dola
na wizara hizo kuachwa.
“Naona kama kulikuwa na namna fulani hivi ya
kulindana. Uamuzi wa Bunge ulifikiwa kutokana na msukumo wa wananchi wa
kutaka kujua hatima ya suala la escrow na IPTL, wahisani kusitisha
msaada kwa sababu ya uchotwaji huo wa fedha pamoja na siasa, hasa
zinazolenga urais mwaka 2015.”
Jaji Warioba alisema katika ripoti ya CAG na PAC,
wametaja ukiukwaji wa malipo ya kodi ya ongezeko la mtaji (capital gain)
na ushuru wa stempu (stamp duty) na kuwa wanaohusika katika hilo ni
Wizara ya Fedha na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na upande mwingine
ni Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) ambao uko chini ya
Wizara ya Viwanda na Biashara.
Alisema wanaotakiwa kuidhinisha ulipwaji wa kodi
ni TRA, huku akihoji kitendo cha ripoti hizo mbili kuonyesha hisa
zimeuzwa kwa Sh6 milioni wakati ilikuwa ni Dola 6 milioni, nyingine
kuuzwa kwa Dola 300,000 za Marekani wakati ilikuwa Sh20 milioni.
“Hapa kuna ufisadi, maana hata kampuni iliyotajwa
kuwa imesajiliwa Brela inaonyesha katika ripoti kuwa wahusika
walioisajili hawakuweka majina yao, waliweka saini tu,” alisema.
Alisema uamuzi wa Bunge uliilenga Wizara ya
Nishati na Madini lakini hasara iliyotajwa kuonekana inazihusu zaidi
Wizara ya Fedha na ile ya Viwanda.
“Kulikuwa na mchezo wa siasa, kwamba baadhi
walindwe na wengine waachwe. Taarifa ya kamati imesema Kampuni ya PAP
kwa kushirikiana na ofisa wa ngazi za chini wa TRA walidanganya. Hivi
suala la kudanganya linafanywa na maofisa wa chini tu, kwani wa juu
hawahusiki?”
Alisema kama ilivyokuwa kwa Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda kutakiwa kujiuzulu kwa maelezo kuwa alikuwa akifahamu mlolongo wa
wizi huo, hata Hazina ilitakiwa kubanwa kwa sababu nayo ilikuwa
ikifahamu suala hilo... “Tumeambiwa kuna uchunguzi unafanyika. Jambo
hili bado halijafikia mwisho, iweje wengine waachwe wakati imeonekana
wazi kuwa Serikali imepata hasara?”
Waliopata mgawo
Jaji Warioba alisema suala jingine lililokosa
majibu ni kitendo cha watu wanaodaiwa kupewa fedha na James Rugemalira
kutajwa majina yao sambamba na akaunti ya aliyewapa, lakini wale
waliodaiwa kuchota fedha hizo katika magunia hawakutajwa
إرسال تعليق