BLACK KOPA CHANGAMOTO MPYA KWA WAIMBAJI WA KIUME WA TAARAB

Black Kopa ni mmoja wa waimbaji wa kiume wa kundi jipya la Ogopa Kopa Classic Band ambaye amekuja na ladha ya aina yake ya uimbaji.
Ni mtoto wa malkia Khadija Kopa, mdogo wake na marehemu Omar Kopa, lakini kwa namna alivyojaaliwa sauti nzuri, hana hata haja ya kusafiria nyota ya mama yake au kaka yake. Anajitosheleza yeye mwenyewe.
Ukisikiliza wimbo wake “Full Ku-enjoy” utakubali kuwa Black Kopa ni changamoto mpya kwa waimbaji wa kiume wa taarab.
Katika moja ya mazungumzo yake na Saluti5, Black Kopa ambaye jina lake halisi ni Muhammed Kibwana, alisema ameingia kwenye ‘game’ kwa miguu yote miwili na hivyo mashabiki wa muziki wa taarab watarajie mengi kutoka kwake.
“Full Ku-enjoy” ni utunzi wake Hemed Omar wenyewe wanamwita Sonara wa maneno.
Hebu thibitisha ubora wake kwa kusikiliza hapo chini wimbo wake wa “Full Ku-enjoy”

Post a Comment

أحدث أقدم