Dar es Salaam. Baada ya saa 24 kupita tangu
kundi maarufu la waporaji la Panya Road, kuvamia na kusababisha shughuli
mbalimbali kusimama kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, chanzo cha
uhalifu huo kimebainika.
Hali hiyo iliwafanya wakazi wa jiji hilo kusitisha shughuli mbalimbali kutokana na kuhofia usalama wao, huku usafiri ukiadimika.
Tukio hilo linaelezwa lilitokea ikiwa ni ishara ya
kundi hilo kumuenzi mwenzao aliyefikwa na mauti akidaiwa kutaka kuiba
pikipiki.
Mkazi wa Magomeni Kagera, Mohamed Chalamira
alisema, “Wakati wakitoka kuzika walikuwa wakiambiana kuwa mwanajeshi
hawezi kuuawa na kuzikwa bila kupigwa mizinga hivyo tutakwenda
kulianzisha ili polisi wapige mabomu na ndicho kilichotokea.”
Aliongeza: “Ni tukio lililotuacha tukishangaa,
kwani polisi mmoja aliyekuwa na silaha alitaka kumkamata mwenzao, lakini
alipotoa panga tu yule polisi alikimbia, hii haiwezekani yaani polisi
anakimbia mhalifu? Ilikuwa saa 9 vijana waligeuza eneo hilo (Magomeni
Kagera) kama eneo lao.”
Kuhusu vijana waliokamatwa Chalamira alisema: “Hao
vijana wawili waliokamatwa mmoja kweli anahusika, lakini mwingine ni
hahusiki kwani dereva, huyo mshikaji atasota huko wakati hahusiki,
polisi wafanye uchunguzi wao kwani haiwezekani kundi hili likasababisha
mtafaruku...Mimi mwenyewe juzi nimepoteza simu na nimeumia hapa katika
goti.”
Familia yazungumza
Kaka mkubwa wa marehemu, Mohamed Ayubu maarufu
‘Diamond’, Moshi Hamadi alisema mdogo wake huyo alizaliwa mwaka 1995
Magomeni Kagera na kukulia kwenye familia hiyo, lakini aliondoka
kutokana na tabia zake kuanzia kubadilika.
Alisema Ayubu hakubahatika kumaliza elimu ya
msingi kutokana na kujiingiza katika makundi ya wavuta bangi akiwa
darasa la nne na alipoonywa hakukubali na alichukia na kuamua kuondoka
nyumbani kwao.
“Huyu alikuwa ni mtoto wa pekee kwa mama yake,
hakuwahi kupata mtoto mwingine, ndiyo maana hawezi kuzungumza presha
imempanda,” alisema Hamad baada ya mwandishi kuomba kuzungumza na mama
yake mzazi na alijibiwa hivyo.
Kauli ya Hamadi iliungwa mkono na mama mkubwa wa
marehemu Ndam Moshi ambaye alisema Ayubu hakutaka vitendo vyake
vijulikane na alipokuwa akienda kuwasalimia walipomgusia kwamba siku
hizi anajihusisha na masuala ya wizi alikuwa anakataa na kulia kutwa
nzima.
Kuhusu taarifa za kifo chake, Hamadi alisema
walipigiwa simu na vijana wasiowafahamu kuwataarifu kuwa Diamond
amefariki dunia kwa kukatwa mapanga eneo la Tandale kwa Mtogole ambako
kulikuwa na mkesha wa Mwaka Mpya
إرسال تعليق