Saluti
kwa wanangu wote tunaochekiana kwa mafoni deile kupeana madini ya
kuwalisha masela. Inakuwaje kwa kitaa hiyo ya bee machalii? Ni mpango
mzima? Selaa huku kwa fasi ya tauni Bongo tambarare watu tunakabana
makoo ileile. Ilimradi tu mwisho wa dei vichwa visomeke. Ama nini? Kaa
humu wewe uwe mjanja wangu.
Ebana tudei no mboyoyo mingi kozi laifu liko resi hatare. Kuna
mwanangu Chuma au Benz ana bonge la talenti kwenye gemu la miyuziki bati
anazingua kinoma! Hataki kukubali kwamba anatakiwa kuchukua makomenti
ya vichwa vyake vyenye lavu na yeye dheni kudili nayo ili kusevu laifu.
Nimemaliza. Atakuwa amewasoma machalii!
Turudi kwenye mastori moo ya hapa jamvini. Huku na huku nimemingo na
kichwa changu Frank niliyemanyana naye kitambo bati tukalostiana. Si
unajua tena mbishe za kutafuta laifu? Huyu akiingilia huku mwingine
anatokea kule hadi kieleweke.
Miaka ilikuwa imekwenda fasta ileile. Ghafla baba la baba huyu hapa.
Mwanangu ananigonga na mkasa wake noma sana aliokutana nao kipindi
tumepotezana kwenye sayari hii ya dunia.
Jamaa ananiteli kwa mahasira kuwa baada ya kulostiana tulipomaliza
skuli, alipata mbebi mkareee… Akaona ili amuwini ni beta akamtwanga na
kitu cha mereji ili ajihakikishie umiliki. Si unajua zile za kufolu
inilavu mzimamzima?
Msela hakuwa mtu wa kuseto mahomu, alikuwa anasafiri mara kibwena
kozi mbali na kupiga mbishe za jobu pia ni bizinesmani.Wani dei msela
alirejea maisha plasi naiti kali akiwa ametokea kwenye mabizinaa.
Kidume akagonga maskani kwake, akafunguliwa na beki tatu dheni akazama ndani kwa mbwembwe kinoma.
Kidume akagonga maskani kwake, akafunguliwa na beki tatu dheni akazama ndani kwa mbwembwe kinoma.
Kaka mkubwa hakuamini alichokiona kwani alimkuta msela f’lani
kisharobaro cha kitaa akiwa na mai waifu wake kwenye bedi wakifanya
yao.Unajua kilichohapeni mazee? Kaa hapo. Unaambiwa mwana alijiona
mnyonge kozi aliishiwa nguvu, hakuwa na mkwanja wa kulipiza na hata
mkwara hakuwa nao. Chezea kuibiwa mali zako? Moyo nao una nyama siyo wa
chuma so unauma.
Alichokifanya kachaa wangu ni kusepa homu huku akimwachia maza watoto
wake kila kitu dheni yupo tauni ameanza laifu upyaaa.Unajua wanangu
kuna sampo za makiksi wa kumeri na wengine ni wa kuruka viwanja tu siyo
waifu matirio. Sasa mameni wengi wanamaindi kumingo na mashori wakare
bila kujua kwamba si wa kumeri. Unakwendakwenda tu bila daireksheni?
Itakula kwako mzazi.
Ukicheki kiundani ishu ya mwanangu Frank utanotisi kwamba naye
alikimbilia kuoa tu kwa kuwa aliona mtoto mzuri pale kati na rangi
adimu. Fulu kuzinguka na mchuchu mkare aibu. Ona sasa anaungaunga na
ameshalosti taimu kinoma. Washkaji si mnajua laifu halirudi nyuma? Taimu
ikikatika ndo kama hivyo hairudi baki.Ebana eee…wanangu mmenisoma?
Ungekuwa wewe ungefanyaje? Tafakari dheni chukua hatua!
Kama vipi sii yuu neksti wiki. Nduki!
Kama vipi sii yuu neksti wiki. Nduki!

إرسال تعليق