Wasafirishaji wa magari ya abiria mkoani tanga wawakalia kooni wasafirishaji abiria kutoka Kenya kwa kukwepa kodi.


Wasafirishaji wa magari ya abiria mkoani tanga wameiomba serikali kuchukua hatua haraka kudhibiti baadhi ya wasafirishaji kutoka nchi jirani ya kenya kuingia nchini kisha kubeba abiria bila kulipa kodi kwa serikali hatua ambayo ni ukiukwaji wa sheria za usafirishaji za kimataifa.
Wametoa ombi hilo kwa viongozi wa serikali ngazi ngazi ya mkoa wa tanga,jeshi la polisi na mamlaka ya udhibiti,usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA) katika kikao cha pamoja cha kujadili changamoto zinazowakabili wasafirishaji na kusababisha matukio ya ajali za barabarani kushindwa kudhibitiwa.
 
Wameilalamikia halmashauri ya jiji la tanga kwa kuruhusu wasafirishaji wenye magari yaliyosajiliwa namba za kenya kuegesha mabasi yao katika baadhi ya hoteli jijini tanga kisha kuwaamuru wasafirishaji wazawa kwenda katika kituo kikuu kipya cha kange ili wenzao wa waweze kuchukua nafasi ya kufanya kazi kwa tija katikati ya jiji bila kulipa kodi kwa serikali.
 
Akielezea hatua hiyo kaimu mkurugenzi wa barabara wa mamlaka ya udhibiti,usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA) Bwana Leo Ngowi amepiga marufuku wenye mabasi hayo kukiuka sheria za usafirishaji za kimataifa na kutishia kuyafutia leseni za usafirishaji wa kuja nchini endapo wataendelea kukiuka sheria na taratibu zilizowekwa.

Post a Comment

أحدث أقدم