Machi mwaka huu Chama cha Mapinduzi (CCM) kinatarajia kuanza
rasmi mchakato wake wa kura ya maoni ya kuwapata wagombea wa nafasi za
ubunge na udiwani watakaopeperusha bendera ya chama hicho kwenye
Uchaguzi Mkuu.
Wahenga walisema kufanya kosa siyo kosa bali
kurudia kosa. Katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji
wa mwaka jana tumeshuhudia CCM kikifanya makosa na sasa kinayajutia.
CCM ilifanikiwa kupata ushindi wa jumla wa mitaa
na vijiji 9,406, kwa pamoja vyama vingine vya upinzani, viligawana
nafasi 3,211.
Kwa ushindi huo upinzani umeongeza viti 1,981
ikilinganishwa na uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliopita wa mwaka 2009
ambao kwa ujumla, ulipata nafasi 1,230 za wenyeviti wa mitaa na vijiji.
Kwa upande wake, CCM imepoteza nafasi 2,636 za
uenyekiti wa vijiji na mitaa ikilinganishwa na uchaguzi wa mwaka 2009
ilipopata jumla ya viti 12,042.
Machi mwaka huu CCM inatarajia kuanza mchakato
wake wa kupata wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi
watakaosimamishwa kupambana na wale wa upinzani katika kuwania nafasi za
ubunge, udiwani na hata urais.
Tumeshuhudia pilikapilika za kujipitisha kwa
baadhi ya makada wenye nia ya kuwania nafasi hizo, lakini ukweli ni
kwamba CCM inapaswa kuhakikisha kwamba hairudii tena kufanya makosa
yaliyowanufaisha wapinzani.
Makosa ya CCM yalipoanzia
Makosa hayo ya CCM yalianzia kwenye mchakato wa
kura za maoni na malalamiko ya wanachama wake yalihusu kutopitishwa kwa
viongozi waliowataka, badala yake baadhi ya viongozi kutaka kutimizwa
kwa matakwa yao binafsi.
Msemo wa umoja ni nguvu utengano ni dhaifu, hapo
ndipo ulipodhihirika baada ya baadhi ya wanachama kuamua kujitenga
kuunga mkono na kusaidia kampeni na badala yake wakaanza kuchafuana na
hatimaye kutoa mwanya kwa wapinzani kushinda.
CCM ingawa imeongoza kwa kupata idadi kubwa ya
viti hivyo, bado matokeo hayo yanabaki kuwa changamoto kubwa kwa sababu
viti vilivyochukuliwa awali vilikuwa chini ya CCM.
Kumbe picha iliyopo hapa ni kuwa kama wapinzani
watajipanga vyema, wana uwezo wa kuongeza zaidi majimbo kama
walivyofanya katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
- Soma Zaidi Mwananchi Hapa
- Soma Zaidi Mwananchi Hapa
Post a Comment