NGULI
 wa filamu za Kibongo, Davina Yahaya ‘Davina’, amesema kamwe hatokuja 
kusahau mateso aliyowahi kuyapata akiwa Gereza la Segerea ambapo alikaa 
kwa siku tatu.
Nguli wa filamu za Kibongo, Davina Yahaya ‘Davina’.
Akipiga stori na Uwazi, Davina alisema tukio hilo lilitokea mwishoni 
mwa mwaka 2012 ambapo ilikuwa ni tatizo la kifamilia lililosababisha 
kutupiwa huko japokuwa hakuweza kuliweka hadharani kwakuwa bado lipo 
mikononi mwa sheria.
“Huwa natokwa machozi na kamwe sitokuja kusahau mateso niliyoyapata 
Segerea. Nilikuwa kwa siku tatu lakini niliona kama mwezi, hali ya hewa,
 sehemu ya kulala zilikuwa mbaya sana, wingi wa watu na sikupata hata 
nafasi ya kulala zaidi ya kukesha nikilia,” alisema Davina.
إرسال تعليق