Anwar Ibrahim
                    
                
Hatima
 ya kiongozi wa upinzani nchini Malaysia Anwar Ibrahim ni mwezi march 
mwaka huu iwapo atafungwa jela ama kuwa huru dhidi ya mashtaka yake ya 
ulawiti.
Mahakama kuu ya Malaysia inatarajiwa kupitia rufani ya 
Anwar aliyekutwa kutwa na makosa ya kufanya mapenzi ya jinsia moja na 
msaidizi wake wa kiume mwaka 2008.
Hata hivyo Anwar mwenyewe 
anasema kuwa mashtaka haya dhidi yake ni sehemu ya kampeni za kisiasa 
kutaka kumpunguzia hadi yake zinazofanywa na chama tawala cha UMNO.
Anwar
 aliyekuwa naibu waziri mkuu wa Malaysia miaka ya 90 alijiunga na 
upinzani,na alifungwa jela kwa miaka sita baada ya kubainika na makosa 
ya ufisadi na mapenzi ya jinsia moja kabla ya mashtaka mengine kama hayo
 yaliyomkumba kwa mara ya pili.(BBC)

إرسال تعليق