Viongozi wa Dini Waaswa kutotumia MAKANISA Yao kunadi Wagombea

VIONGOZI wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini wametakiwa kuacha tabia ya kuwakumbatia na kuwanadi baadhi ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi mbele ya waumini wao kwa kutumia nyumba za ibada.
 
Rai hiyo ilitolewa jana mjini Songea na Mwenyekiti mpya wa Serikali ya Mtaa wa Making’inda, Hashim Asham alipokuwa akizungumza na wanawake wa mtaa huo wakati wa uzinduzi wa Chama cha Akiba na Mikopo (Saccos) ambapo pia amewasihi viongozi hao kuahamasisha waumini wao kujitokeza kuipigia kura Katiba Iliyopendekezwa.
 
Alisema baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa na tabia ya kuwafanyia kampeni wagombea wanaowataka wao, jambo linaloweza kuibua mitafaruku mikubwa katika nyumba za ibada.
 
Alisema viongozi hao wamekuwa wakijihusisha na siasa huku wakitumia nyumba za ibada na kushabikia waumini kuchagua aina fulani ya wagombea, jambo alilosisitiza ni kinyume cha maadili ya kazi zao.
 
Katika uzinduzi huo uliohudhuriwa pia na viongozi wa dini, alisema viongozi wa aina hiyo hawajui wanachokifanya, kwani wanaacha majukumu yao ya msingi badala yake wanaingilia kazi za watu wengine na yanaweza kuwagharimu kwani kuzomewa au matusi ni jambo la kawaida kwa wanasiasa, lakini sio kwa viongozi wa dini.

Post a Comment

أحدث أقدم