Serikali
 imehadharishwa juu ya uvamizi na wizi wa silaha katika vituo vya 
polisi, kwa kuambiwa hali hiyo inatisha na kuhitaji hatua za makusudi 
kuimarisha ulinzi nchini. 
  
  
  
  
  
  
  
  
  
  
  
  
Aidha,
 ilishauri polisi kwa kushirikiana na jamii iongeze jitihada na ibuni 
mbinu mpya za kudhibiti wale wote wanaoendesha uhalifu na uuaji wa watu 
wenye ulemavu wa ngozi na vikongwe.
Baadhi
 ya wabunge wameshauri Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na
 Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), yaruhusiwe kusaidia Polisi kulinda raia 
na mali zao, hususan kudhibiti vikundi vya kihalifu vinavyojitokeza. 
Akichangia
 taarifa ya Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama iliyowasilishwa 
bungeni, Mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan (CCM) alisema vituo vya polisi 
kuvamiwa na majambazi na kuibiwa silaha, ni hali inayotisha 
ikidhihirisha uhalifu ulivyokithiri nchini.
“Tuyaombe
 majeshi mengine ya ulinzi ya nchi yasaidie jeshi la polisi. Kama 
tuliweza kutumia majeshi mwaka jana kupambana na majangili, leo 
tunashindwa nini kupambana na wahalifu hawa waliokithiri?
“Si
 dhambi kutumia askari wa JWTZ au JKT kulinda nchi yetu. Eti wanajeshi 
wetu wako nje ya nchi wanalinda wananchi, lakini ndani ya nchi yetu 
wananchi wanaumia.”
Alisema
 magenge ya kihalifu, wizi na uhalifu unaojitokeza unatisha sana. Alitoa
 mfano wa kuibuka kwa kikundi cha Panya Road jijini Dar es Salaam na 
kusema askari ama kwa uchache au kwa kukosa vitendea kazi, wanashindwa 
kudhibiti uhalifu.
Alitoa
 mifano mingine ya uhalifu ni pamoja kukithiri kwa wizi wa kutumia 
pikipiki na kusema imefikia hatua, watu wanaoporwa wameviona vitendo vya
 kawaida kwa kutokwenda kuripoti polisi. 
“Kama
 hatuwezi kuajiri askari wa kutosha kwenye jeshi la polisi tukawapa 
vitendea kazi jeshi la polisi, wakapewa makazi bora, ulinzi au usalama 
utakuwa katika hali ya hatari huko tuendako,” alisema. 
Akihimiza majeshi kutumika kudhibiti makundi ya kihalifu yanayojitokeza kwenye jamii, mbunge huyo alisema, "Majeshi,
 hasa JKT wako vijana wengi kambini. Kwa nini tusiwatumie? Tunaona shida
 gani kuwatumia? Si suala la kukaa na kusema, kimataifa jeshi 
hawaruhusiwi kulinda.” 
Awali,
 Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama, katika taarifa ya utekelezaji wa 
majukumu yake kati ya Februari mwaka jana na Januari mwaka huu, ilisema 
ilibaini katika kipindi hicho hali ya ulinzi wa nchi na usalama wa raia 
ilikuwa shwari.
Kamati kupitia kwa Mjumbe wake, John Chiligati ilipongeza jeshi la polisi kwa jitihada  za kudhibiti uhalifu nchini.
“Kamati
 ilipotembelea Mkoa wa Arusha iliridhika na hali ya kupungua matukio ya 
uhalifu na pia ilikuta hali ya utulivu na amani imerejea katika Jiji la 
Arusha,” alisema Chiligati. 
Hata
 hivyo, kamati ilishauri polisi itafute njia mbadala na za kisasa za 
kupambana na kudhibiti uingizaji nchini wa dawa za kulevya, ukiwemo 
usafirishaji bangi kwenda Kenya na uingizaji mirungi nchini kutoka 
kutoka nchi hiyo. 

إرسال تعليق