Wamachinga Ubungo waing'aka Manispaa

Wamachinga Ubungo
Umoja  wa wafanyabiashara ndogo ndogo Ubungo jijini Dar es Salaam, wameujia juu uongozi wa Manispaa ya Kinondoni kutokana na vitendo vya kufukuzwa na kunyang’anywa bidhaa zao kabla ya manispaa hiyo haijawatafutia maeneo mengine ya kudumu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa umoja huo, Honoratha Mashoto, alisema Manispaa ya Kinondoni iliahidi kuwapatia eneo la Simu 2000 kwa ajili ya kufanyia biashara zao.
“Hatupendi kuhangaika barabarani na kupambana na mgambo wa Manispaa mara kwa mara kama raia huru wa nchi hii na wala si wakimbizi kwenye nchi yetu. Tunaomba tuwe na kituo rasmi na cha kudumu cha kuendeshea biashara zetu kwa amani na utulivu na siyo kukimbizana kila siku,” alisema.
Alisema wanamuomba waziri mwenye dhamana aishinikize Manispaa ya Kinondoni kutumia eneo la ekari nne zilizobaki kwenye kiwanja Na. 2005/2/2. Kitalu  ‘C’ Sinza eneo la Simu 2000 kinachomilikiwa na Halmashauri ya Manispaa kwa ajili ya wafanyanyabiashara ndogo ndogo.
Hata hivyo, Msemaji wa Manispaa ya Kinondoni, Sebastian Mhowera, alisema hautambui umoja huo kutokana na kufanya biashara sehemu  zisizo rasmi

Post a Comment

أحدث أقدم