He
he he heeee, acha nicheke miye mwana Kibatari mjukuu ya Kandili, unajua
vitu vingine vinachekesha kama si kusikitisha, unalalamika mwanamke
mzima uliyekamilika tena bila aibu eti mfanyakazi wako wa ndani anakulia
mali zako kwa mumeo kuhamishia mapenzi kwake!
Unajua kauli hiyo hunifanya nikumbuke ile kauli isemayo mpambe awe
mwenye mali na mwenye mali aonekane mpambe. Ooh, nilikuja na kasi ya
ajabu na miye bila salamu kwa kuwahi kuzima moto ambao sasa hivi
umetanda kila kona ya nyumba zetu hasa wafanyakazi ambao wameolewa na
kumuweka msaidizi wa ndani yaani house girl.
Kutokana na kuwa na mfanyakazi wa ndani basi kila kitu unamuachia
akifanye, ambacho ni makosa kwa mwanamke aliyefundwa akafundika kumuacha
mfanyakazi wa ndani amfanyie mumeo kazi zinazokuhusu!
Tangu lini fisi akaachiwa bucha wewe na mfanyakazi wako wa ndani
mnazidiana nini kimaumbile, pengine mfanyakazi wako Mungu kampendelea
kuliko wewe. Kwa vile unafanya kazi basi ukirudi unautupa mkoba wako
unakwenda kuoga, ukila unapanda kitandani kutokana na uchovu wa kutwa
nzima.
Unamwacha mfanyakazi wa ndani afanye kazi zote kumsubiri mumeo wewe
umelala akirudi amtengee maji ya kuoga wewe umelala amtengee chakula
huna habari unajigeuza kitandani. Anaondoa vyombo pengine amevaa upande
wa kanga bila kitu ndani na kama anajua yupo katika mkao wa kula naye
hufanya vibweka vya kuchezesha makalio na kuacha matiti nje.
Sehemu hizo ndizo huwatoa imani wanaume na kujikuta akijaribu kwa
vile naye ana hamu zake basi shoga wee unalala watu wanajilia vyao.
Ulikuwa wa kuamshwa usiku.
“Honey leo nimeshikwa mwenzio.”
“Honey leo nimeshikwa mwenzio.”
Unajikuta unalala kila siku bila kuguswa kutokana na uchovu wa kazi
unaona sawa kumbe nyani kaingia shambani wee wapiga usingizi mali zako
zinaliwa. Leo na kesho mfanyakazi wako wa ndani anageuka mke mwenzio
tena mapenzi yote mumeo anayahamishia kwa mfanyakazi kwa vile ndiye
anayemfanyia zaidi ya mke.
Utakalia kulia “Aah, nyani kavamia shamba langu naanza kuvuna mabua,” we mwenyewe umemchekea nyani acha uvune mabua.
Shoga nataka nikueleze sheria za ndoa hata kama unafanya kazi gani
hakikisha baadhi ya vitu hasa vimuhusuvyo mumeo mfanyakazi wa ndani
havigusi. Kufuliwa nguo, kutengewa maji ya kuoga kula lazima ale mumeo
ukiwa pembeni hata kama umeshiba basi mlishane hata tonge mbili.
Mumeo ni lulu isiyotaka kuguswa na mtu, itunze kwa nguvu zako zote,
hakikisha hakuna mtu atakayeigusa hata shoga yako ila wewe mwenyewe.
Mfanyakazi ana mipaka yake wala asiwe na mazoea kwa mumeo.
Narudia wewe na mfanyakazi hamkupishani kitu kila ulichonacho anacho
ana matamanio na yeye vilevile anataka vitu vizuri. Kufanya kazi
usijisahau na kuona kazi ni bora kuliko mumeo, kazi ina umuhimu kwa
sehemu zake na ukifika nyumbani mwenye nafasi ya pekee ni mumeo,
kuhakikisha anapata huduma zote muhimu kutoka kwa mkewe.
Kinachowaumiza wanawake wengi ni uvivu hasa wanapokuwa wanafanya kazi
na kumuachia fisi bucha unategemea nini kama siyo kukuta amekula mpaka
gogo la kupasulia mifupa.
Yangu nimemaliza, la muhimu kuyafanyia kazi la sivyo utaachika na nyumba unaipenda
Yangu nimemaliza, la muhimu kuyafanyia kazi la sivyo utaachika na nyumba unaipenda

Post a Comment