PICHA 6 ZA ISHA MASHAUZI ALIPOKWEA JUKWAA LA JAHAZI JUMAPILI ILIYOPITA …ukumbi ukazizima …ni amsha amsha za show yao ya Machi 22

Jumapili iliyopita mkurugenzi wa Mashauzi Classic, Isha Mashauzi alikwea jukwaa la Jahazi Modern Taarab na kuleta msisimko wa aina yake.
Isha ni msanii aliyechipuka na kuwa maarufu kupitia Jahazi Modern Taarab kabla hajaamua kuanzisha bendi yake miaka minne iliyopita.
Mara tu Isha alipopanda jukwaani sambamba na Mzee Yussuf mashabiki wakalipuka kwa furaha na kukumbukia vitu vyake adimu alivyovifanya ndani ya kundi hilo.
Isha alitumia muda wake jukwaani kunadi onyesho la pamoja la Jahazi na Mashauzi litakalofanyika Travertine Hotel Magomeni Jumapili ya tarehe 22 mwezi huu.
Akawapa vionjo vifupi vifupi vya nyimbo zake kadhaa ukiwemo “Yawenzenu Midomoni” aliouimba akiwa na Jahazi.
Mashabiki wakalipuka kwa furaha na kumtaka aimbe wimbo huo lakini yeye na Mzee Yussuf wakawaambia mashabiki hao wavute subira na wasipunguze utamu wa Machi 22.
 Mzee Yussuf (kushoto) akisisitiza jambo na Isha Mashauzi (katikati)
 Isha akipagawisha kwa vionjo vyake
 Shabiki akienda mtunza Isha jukwaani
Mtu na mwanae walivyopendeza jukwaani
Baada ya kushuka jukwaani bado Isha na Mzee waliendelea kujadiliana mambo kadha wa kadha
 Mjadala wa hapa na pale ukiendelea

Post a Comment

أحدث أقدم