Mastaa wa Bongo Fleva,Q-Chillah na TID mwishoni mwa wiki hii walitaka kutwangana walipokutana katika Klabu moja usiku.
 
Kwa mujibu wa Q-Chillah akizungumza kwenye Uheard na Soudy Brown alisema kuwa alikwenda kwenye klabu hiyo kuangalia shoo iliyokuwa ikifanyika lakini baadaye aliamua kutoka nje kucheza ‘pool table’ ndipo alipomuona TID.
Kwa mujibu wa Q-Chillah akizungumza kwenye Uheard na Soudy Brown alisema kuwa alikwenda kwenye klabu hiyo kuangalia shoo iliyokuwa ikifanyika lakini baadaye aliamua kutoka nje kucheza ‘pool table’ ndipo alipomuona TID.
‘’Nilimuona jamaa(TID) akiniangalia na baadaye 
alinifuata akaniambia kuwa anataka kuongea na mimi nikamwambia ile siye 
sehemu yake atafute muda mwingine ndiyo tuongee,’’alisema Q-Chillah. 
Aidha Chillah aliongeza kuwa TID aliendea kumuongelesha 
ndipo alimwambia kuwa anachofanya kumuongelea yeye vibaya siyo vizuri na
 kile alichokipost hivi karibuni kuhusu kuuponda wimbo mpya wa msanii 
Ali Kiba uitwao ‘Cheketua’ aliouachia hivi karibuni kupitia account yake
 ya Instagram hakikuwa kitu cha busara ilitakiwa amsapoti kama msanii 
mkongwe kuliko kumponda hadharani kupitia mitandao.
‘’Kiukweli kitendo cha TID kuandika Instagram kuwa ngoma mpya ya 
Alikiba ni mbaya na baada ya miezi mitatu haitokuwepo siyo kizuri 
nilimwambia yeye ni msanii mkubwa inabidi kumsapoti Ali Kiba na kwamba 
nilitaka kumpiga kwa fimbo ya pool table siyo kweli nilikuwa nikimueleza
 tu,’’aliongeza Q-Chillah.
Kwa muda mrefu wasanii hao wawili ambao waliwahi kuwa 
pamoja kwenye bendi ya (Top Band) wamekuwa kwenye bifu zito wakitupiana 
maneno kwenye vyombo vya habari.

إرسال تعليق