HOJA BINAFSI: Mabloga zingatieni maadili kuheshimu picha za marehemu mitandaoni

Raha ya kipindi tunachoishi sasa  ni wepesi wa mawasiliano. Mawasiliano ya haraka kwa simu za mkononi, habari kusambaa, mitandao kutupasha yaliyotokea, ghafla bin vuu. Hakuna  linalofanyika hadharani likapita, vuum,  siku hizi. Iwe umbea au udaku; serikali, mazuri au kashfa, gharika au tufani; ili mradi...Buum! Hiyo hapo machoni.
Hata mambo ya binafsi ambayo miaka 25 iliyopita yaliwekwa uvunguni. Ya mtoto kuzaliwa, mtu kuonyesha chakula alichokila, wanawake kutangaza madoido na  urembo wao wa kucheza na kukata viuno, nk. Tunaishi msimu wa majigambo ya nafsi. Kutaka kuonekana, kusifiwa  kujinadi  hadharani; kwa uzuri au ubaya. Kila mtu ajue.
 Kiingereza kina neno lake maalumu la kifalsafa.
 “Narcissism”....lenye asili Uigiriki. Enzi Wagiriki wakitawala maendeleo (kama Marekani leo)  Narcissus, kijana wa kiume aliyekuwa na haiba maridadi, alijienzi kiasi ambacho siku moja Nemesis mwanamke wa kuvutia, akamghilibu ajitazame katika  dimbwi la maji. Narcissus alivyokuwa na huo upendo wa wajihi wake alikaa pale akijifurahia alivyokuwa mrembo.  Kumbe ule wasifu aliouona majini ulikuwa picha tu. Njozi.
Sasa  Narcissus akawa anapotelea ndani ya hiyo njozi ya wajihi wake, akijifurahia hadi alipojisahau na kuanguka dimbwini. Akafa. Ndiyo maana ipo nahau ya Kiingereza isemayo “he met his nemesis” au “she met her nemesis”...yaani, mtu unakutana na Ibilisi au jambo linalokuweza na kukuangamiza.  Nemesis alimtega na kuchangia kuaangamia kwa Narcissus si kwa ubaya ila kutokana na kujipenda kuzidi kawaida.
Mantiki ya kisa inatufundisha nini kuhusu lugha, maisha na maudhui?
Tuko ndani ya mazingira ya kupenda umaarufu na kujitangazia lolote tunalolifanya na kulishirikisha kwa yeyote yule. Ndani ya mazingira yetu mna hulka ile ya methali ya Kiswahili, “ Hapana siri ya watu wawili...”
Raha imo, ndiyo.  Kufichua mabaya. Polisi weupe wa Kimarekani sasa hivi wanakosolewa kutokana na vitendo vyao vya kuua watu weusi waliovunja sheria mitaani bila kuwafikisha mahamakani. Siyo kwamba ni mambo mapya. Tangu enzi magenge ya weupe yakiwavizia watu weusi na kuwanyonga hadharani kwa kosa dogo la kutongoza msichana wa Kizungu. Yalitendeka. Tofauti? Leo huwekwa hadharani kutokana na vifaa kama simu za mkononi na video zilizozagaa barabarani majuu (CCTV).
Raha ya mablogu ndiyo hiyo.Ufidhuli na ufisadi wa viongozi wapotofu unachojolewa soksi, sidiria na kofia. Kama ilivyotokea vuguvugu za Mashariki ya Kati (Arab Spring): Tunisia, Libya, Misri na kuishia  viongozi waliowatesa wananchi kutolewa madarakani. Kifo katili cha Kanali Muammar Gadaffi mwaka 2011 mathalan, kiliwekwa wazi.  Uanahabari wa kijamii kilingeni.
Hapa kwetu Tanzania mwanahabari wa TV, Daudi Mwangosi alipouawa kinyama mwaka 2012, picha ya viungo vyake  vya ndani (utumbo na kadhalika) ziliwekwa wazi wazi mitandaoni.  Sasa hivi ukibofya tu Daudi  Mwangosi, vimeselelea  mitandaoni.  Wanablogu walikuwa watu wa kwanza kuonyesha ukatili wa askari walioyateketeza maisha ya Mwangosi akiwa kazini na kuiacha familia yake ikilia mayowe hadi  mtondogoo.
Mabloga ni wanahabari huria
“Houria” ni uhuru  kwa Kiarabu. Uhuria huu uliochipuka mwaka 1990 baada ya kuanguka himaya ya Ukomunisti na kubomolewa ukuta uliotenganisha Ujerumani ya Mashariki na Magharibi, mjini Berlin. Mengi yaliyofuatia hapo yameweka utamaduni wetu sasa. Kufunguliwa Nelson Mandela kutoka jela baada ya miaka 26. Akaanzisha serikali mpya iliyo ahueni na kiini  cha safari za Waafrika wengi kushuka Afrika Kusini. Wagonjwa wetu kwenda kutibiwa, ushirikiano wa kibiashara, runinga na vipindi vya TV, nk. Pia kuanzishwa kwa vyama mbalimbali vya kisiasa barani Afrika. Uhuria huu ulituathiri pia katika starehe; tuna muziki wa kizazi kipya ...muziki wa Bongo Fleva. Umejenga ajira kwa vijana wanaojituma,  kutegemea muziki. Kinyume na miaka 35 iliyopita siku hizi tunao wanamuziki matajiri kuliko enzi za marehemu Patrick Balisidja, Mbaraka Mwinshehe, Kiko Kids na Marijani Rajab.  Tuna vyama vya upinzani na wanasiasa chipukizi mathalan Zitto Kabwe na January Makamba. Enzi za Tanu kiongozi kijana alikuwa Chediel Mgonja aliyeingia baraza la mawaziri akiwa na umri mdogo wa miaka 31-33. Haikuwa kawaida na siyo wengi wanamjua Mgonja aliyekuwa Waziri wa Elimu kadhalika. Alipofariki mwaka 2009,  mmoja wa watoa maoni ndani ya blog la Michuzi alisifia:

Post a Comment

أحدث أقدم