MJAMZITO AJIFUNGUA NAZI! ASIMULIA MKASA MZIMA, INATISHA

Maajabu! Msichana aliyefahamika kwa jina la Dora mkazi wa Magomeni Bagamoyo mkoani Pwani, hivi karibuni amejikuta akijifungua nazi badala ya mtoto, jambo lililomshangaza kila mtu.
Ushirikina watajwa
Dora anayedaiwa kujifungua nazi.
Ilidaiwa kuwa, chanzo cha Dora kujifungua nazi ni maneno aliyoambiwa na mke mwenzake aliyefahamika kwa jina la Jamila ambapo aliambiwa hatajifungua kiumbe cha kawaida na ndipo alipokimbilia Dodoma kukwepa matatizo.
Msikie Dora
Akizungumza na Amani hivi karibuni akiwa nyumbani kwake Bagamoyo, Dora alisema:
“Nilihamia Bagamoyo nikitokea Mwanza, nikakutana na mwanaume anayeitwa Pascal, tukakubaliana tuishi kama mke na mume.
“Baada ya kukubaliana hilo, nikapata ujauzito lakini nikashangaa siku moja akaja mwanamke na kusema yeye ni mzazi mwenzake na Pascal.“Alifanya vurugu, akanijeruhi kisha akachukua TV na vitu vingine, akaondoka huku akiniambia lazima nijifungue kiumbe cha ajabu. Nilipata hofu kubwa, mara nikaanza kusumbuliwa na tumbo, nikapelekwa kwa mganga ambapo niliambiwa nimerogwa.
Mume wa Dora akihojiwa na mwandishi wa habari (hayupo pichani)
“Nikatibiwa kisha nikafungwa kitambaa chenye dawa mkononi na kuambiwa nisikivue. “Siku moja kikapotea kimaajabu, baadaye tukakiona juu ya mti nje ya nyumba. Nikaachana na masuala ya kienyeji, nikaamua kwenda kanisani, hata hivyo mauzauza hayakuisha,” alisema Dora na kuongeza:
“Siku uchungu uliponijia nikiwa Dodoma, ndugu zangu na wakunga wakaja kunisaidia lakini cha ajabu wakashangaa kuona nazi ndiyo inatoka.“Wakakimbia na kuniacha nikipandisha mashetani, akaitwa mganga wa kienyeji lakini naye aliogopa ndipo nikapelekwa kwa walokole kuombewa.
“Nilipopata nafuu na kurudishwa nyumbani, polisi wakaja na kutuambia eti tumetupa mtoto, wakasachi hawakuona kitu, wakatupeleka kituoni.“Huko nako nikapandisha mashetani, nilipotulia nikapelekwa hospitali ambako nilisafishwa lakini ishu ikawa kubwa, polisi wakatuchukua mimi na mume wangu na kutuweka ndani, tulitoka baada ya kutoa pesa.
Mfano wa nazi aliyojifungua Dora.
“Cha ajabu niliporudi nyumbani ili nichukue kadi niende kliniki, nikakuta shanga kibao, ndipo tukaona cha msingi ni kurudi Bagamoyo na kuhama pale tulipokuwa tunaishi,” alisema Dora huku akiungwa mkono na mumewe, Pascal.
Imeandaliwa na Chande Abdallah na Deogratius Mongela

Post a Comment

Previous Post Next Post