Niaje…niaje wazazi majembe yangu? Inakuwa nini wanangu wenyewe? 
Kipande hii ni mpango mzima. Hapa ni mwendo wa kubandika na kubandua 
mwanzo mwisho. Ama nene? Mazee kitu cha Pasaka kilihapeni vipi? Dah! 
Siyo sekreti wana mlinifungia vioo bati haina kwere hopu mambo 
yalikwenda flenga. Basi barida!
Ebana eeh…tudei noo kumbwela dheni tunazama kwenye mastori moo fasta 
tuone kama yaliyomo yamo? Shujaa wangu mmoko kakutana na mzinguo hatare 
kinomanoma mazee. Tulia wewe upate hizi ni tamu ileile kudaadeki!
Jamaa bana anakwenda kwa jina la P. Baada ya kupiga kitu cha klasi 
vya kutosha dheni alipata promosheni ya kwenda kupiga mbishe za jobu 
kwenye mkoa f’lani hivi ameizing…kozi ni mkoa wenye laifu tamu kama 
mfukoni uko poa na kweli unapenda mambo ya madevelopumenti.
Basi kaka mkubwa akawa ni kibosile kwenye kampuni moko la ishu za kilimo kwanza.
Selaa akawa anapiga bakora si unajua zile za kiswazi? Pipo wakawa wanampiga chabo tu na swaga zake za mkwara mbuzi watu wanamcheki tu!
Selaa akawa anapiga bakora si unajua zile za kiswazi? Pipo wakawa wanampiga chabo tu na swaga zake za mkwara mbuzi watu wanamcheki tu!
Ebana jamaa akiwa anamingo kitu cha mkoa si ndo akakamata mtoto mkare
 kitu cha kutoka uswazi si unajua tena dhahabu mchangani?Dosari kwa yule
 mtoto mzuri pale kati ni kwamba alikuwa ameshindikana kozi amesharuka 
na mameni kibwena bila kujali masela wa kitaa na washuwa mahazibendi wa 
watu.
Basi msela wangu naye akaingia kwenye kumi na nane za shori akawa 
anajipoozea kwa kula tu wepesi. Jamaa akawa anahudumia kinoma. Mara 
kumpiga usopusopu, bata ndefu na ishu zingine za dizaini hiyo.
Miezi bee tayari mtoto kashiba kitumbo ndii…hihaaa! Hapo ndo mchongo ulipomharibikia mwana kozi aliitwa na maparenti wa shori dheni akasainishwa ili ahudumie!
Miezi bee tayari mtoto kashiba kitumbo ndii…hihaaa! Hapo ndo mchongo ulipomharibikia mwana kozi aliitwa na maparenti wa shori dheni akasainishwa ili ahudumie!
Dah! Huwezi amini msela akajikuta akishikishwa zigo ambalo hakupanga 
kuwa naye kwenye laifu. Wana wanakwambia ndo hivyo mdoli famba ndo huwa 
unauzwa bei ghali kinoma arifu.Miezi bee baadaye si msela akatakiwa 
kurudi makao makuu Bongo tambarare? Unaambiwa maparenti wa shori 
wakaweka kikao cha dharura kuweka ishu pleini.
Walichokuwa wanakompleini maparenti kwamba inawezekana kachaa 
akichomoka asirejee tena hivyo wataumbuka.Walichokifanya maparenti 
wakamfungashia shori akatimua na mwana. Msela alijaribu kufanya kila 
minsi ili kukwepa soo bati likamganda na sasa yupo na zigo bila 
kujiandaa.
Wana mmepata pointi? Samutaim ni beta kujipanga na siyo kwenda resi 
bila kufokasi mbele kujua fyucha itakuwaje? Cheki nawu mwana kapewa zigo
 ambalo hakuwa na taimu nalo tena kapewa na makosti kibwena.
Washikaji mmenisoma? Kama vipi kitu cha wikiendi hichooo…basi sii yuu neksti wiki mazee
Washikaji mmenisoma? Kama vipi kitu cha wikiendi hichooo…basi sii yuu neksti wiki mazee

إرسال تعليق