STAA wa filamu Bongo, Irene Paul ‘Smart Girl’ amezua
mshangao baada ya kupiga mayowe huku akirusha mikono kushangilia tuzo
aliyopata jambo lililozua miguno kwa waliomshuhudia.
Staa wa filamu Bongo, Irene Paul ‘Smart Girl’ akitahayari wakati wa kuchukua tuzo.
‘Katukio’ hako ‘amazing’ kalishuhudiwa na paparazi wetu mwishoni mwa
wiki iliyopita ndani ya Jengo la Mwalimu Nyerere, Posta jijini Dar
kulikokuwa na sherehe ya utoaji Tuzo za TAFA na kuwafanya baadhi ya watu
kuacha kila kitu kwa muda na kumtumbulia macho.
Msanii huyo alipata tuzo hiyo kwa kipengele cha The Best Actress
(Supporting Role) kupitia Filamu ya Never Give Up aliyoshirikiana na
msanii kutoka Nigeria, Joseph Van Vicker na kuonekana kuchanganyikiwa
namna hiyo.
Baada ya kuchukua tuzo hiyo, ‘kiruka njia’ wetu alimfuata na
kumuuliza kulikoni aonekane kupagawa kwa kiwango hicho ambapo alisema
kutokana na ugumu wa kipengele hicho kwani alikuwa akichuana na watu
anaowaheshimu sana katika tasnia ya filamu, alioamini wana kiwango cha
juu kuliko yeye hivyo hakuamini kilichokuwa kinatokea kwa wakati huo.
Post a Comment