KIKAO KATI YA TFF, SIMBA SC, SPUTANZA NA MCHEZAJI SINGANO

Uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo umekutana na
Uongozi wa klabu ya Simba  SC ukiwakilishwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji
Collin Frisch na mchezaji Ramadhani Yahya Singano akiandamana na Uongozi wa
Chama cha Wacheaji wa Mpira wa Miguu (SPUTANZA). Kikao hiki kiliitishwa na
TFF kujadili utata wa kimtakabta kati ya mchezaji na klabu ya Simba.

Katika kikao cha leo pande zote zimeeleza kutambua utata ulio ndani ya
mikataba iliyokuwepo ambayo kimsingi iliingiwa kabla ya uongozi wa sasa wa
Simba SC.

Kwa pamoja pande hizo mbili zimekubaliana kuanza mazungumzo ya makubaliano
mapya na hatimaye mkataba mpya utakaoanza katika msimu mpya wa 2015/16.

TFF imevitaka vilabu kushirikiana na SPUTANZA na Bodi ya Ligi katika kuweka
mifumo mizuri ya uingiaji mikataba.  TFF inao mkataba mama (*template*)
ambao vilabu vyote na wachezaji wanatakiwa waufuate wakati wanaandaa
mikataba yao (*individual contracts between players and clubs*).  Aidha TFF
imewataka  wachezaji kuelewa mikataba kabla ya kutia sahihi.

TFF itazidi kuboresha mfumo wa usajili wa wachezaji na mikataba ili kuweka
mazingira sawia kati ya pande zote mbili (Wachezaji na vilabu)

Makubaliano yamefanyika leo tarehe 9 Juni 2015 na kusainiwa na:-

   - Collin Frisch - Simba SC
   - Ramadhan Singano - Mchezaji
   - Mussa M. Kissoky - SPUTANZA
   - Mwesigwa J. Selestine - Katibu Mkuu - TFF

*IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)*

Post a Comment

أحدث أقدم