MSIMU uliopita Ligi Kuu Bara ilipoanza, Simba ilionekana dhaifu
na yenye tatizo kwa wachezaji wake kukatikiwa pumzi kiasi cha kuwapa
nafasi wapinzani wao ya kuwatawala katika michezo yao.
Karibu kila mchezo waliocheza walitangulia kufunga
bao au mabao lakini mwishowe yalirejeshwa na kufanya timu kuwa na
wakati mgumu mpaka ligi ilipoenda mapumzikoni mwishoni mwa mwaka.
Baadaye Simba iliamua kuachana na Mzambia Patrick
Phiri na kumpa nafasi Mserbia, Goran Kopunovic ambaye, licha ya
kujitahidi kuibadilisha timu, tatizo la ukosefu wa stamina liliendelea.
Pengine kwa kulitambua jambo hilo ndiyo maana
uongozi wa klabu hiyo chini ya Rais Evance Aveva umeamua kufanya jambo
la maana ambalo huenda likawapa wakati mgumu wapinzani wao katika Ligi
Kuu msimu ijayo. Hii ni baada ya kuamua kumleta kocha mkali wa mazoezi
ya utimamu wa mwili (fikizi), Dylan Kerr kutoka Uingereza.
Mbali na umahiri wake wa kuwaweka wachezaji katika
utimamu wa mwili (fitness), lakini ni mahiri wa kufundisha soka la
pasi, jambo ambalo Aveva alitamka wazi kuwa ni kocha waliyekuwa
wakimsaka kwa muda mrefu kuirejeshea Simba heshima yake.
Aveva alisema Kerr ambaye ataingia mkataba wa
mwaka mmoja wenye makubaliano ya kuongezewa mwingine endapo atafanya
vizuri licha ya kwamba hana uzoefu katika nchi za Afrika Mashariki, ila
wanaamini ataibadilisha timu yao kufuatia kuwahi kufanya kazi Afrika
Kusini.
Beki huyo wa zamani wa klabu za Sheffield
Wednesday, Leeds United, Reading na Blackpool zilizowahi kutamba kwenye
Ligi Kuu ya England anatua Msimbazi akitokea Vietnam.
Mchakato
Aveva alianika mchakato wa kumsaka kocha huyo kuwa
ulifanywa kwa umakini mkubwa kabla ya kuafikiana na hatimaye kulazimika
kumuanika hadharani ili kukata kiu ya wanachama na mashabiki wa Simba
waliokuwa wakichanganywa na taarifa mbalimbali za ujio wa kocha wao
mpya.
“Mchakato ulihusisha makocha zaidi ya watano
akiwamo Kim Poulsen aliyewahi kuwa Kocha wa Taifa Stars, lakini
tuliachana naye baada ya kuingiliwa na mambo fulani hasa kwa wakala
wake, na mwishoni turufu ilimuangukia Kerr,” alisema Aveva.
“Tunaamini kwamba Kerr ataisaidia timu yetu kupata
mabadiliko makubwa kuweza kuipa mataji mbalimbali Simba, kazi yetu kama
uongozi ni kumuandalia mazingira mazuri ya kufanya kazi akiwa na
wasaidizi wake.
Usajili
Post a Comment