Video ya Tembo walivyomzuia jamaa na bodaboda yake kukatisha barabarani… (Video)



Wako wanyama kama Simba au Chui ukikutana nao barabarani lazima upate hofu, lakini kama unakatisha zako halafu ukakutana na Tembo unaweza kumchukulia poa, ukamkwepa tu pembeni halafu ukaendelea na safari yako !!
Unajua kwamba kumbe Tembo muda mwingine akikasirika sio mnyama wa kumchukulia poa?!
Video kutoka Thailand, tembo wamekasirika na kumzuia kabisa jamaa ambaye alikuwa anakatisha na pikipiki yake kwenye Mbuga hiyo.. lakini wenyeji wa Thailand wanasema hiyo sio stori ngeni Tembo kuvamia watu wanaokatisha barabara iliyoko kwenye Mbuga ya Khao Yai, mwanzoni mwa mwaka 2015 Tembo aliwahi kuvamia gari na kuiharibu.
Video hii hapa mtu wangu.

Kipande cha Video kingine hiki hapa Tembo alivyovamia gari iliyokuwa inakatiosha Mbugani January 2015.


Post a Comment

أحدث أقدم