Wiki nne za Lilian Miss Tanzania na warembo wengine 120 ndani ya China kuelekea #MissWorld2015




Najua ni kazi yangu kuhakikisha uko karibu na kila stori kubwa mtu wangu, kutoka kona zote… kila inaponifikia na mimi nahakikisha naisogeza kwako !!
Ninayo nyingine ambayo nimefikishiwa kutoka Kamati inayosimamia mashindano makubwa ya urembo Tanzania ambapo safari hii inahusu maandalizi na safari ya kuelekea kilele cha mashindano ya Miss World itakayofanyika December 19 2015 ndani ya Sanya, China.. Mrembo anayeshikilia taji la Miss Tanzania, Lilian Deus Kamazima atakuwa mmoja ya warembo zaidi ya 120 watakaoshiriki fainali hizo.
Lilian Love
Mrembo Lilian Deus Kamazima kwenye picha ya pamoja na Makamu wa Rais Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan.
Ratiba yenyewe iko hivi, mrembo wetu Lilian pamoja na warembo wengine wote watapokelewa China November 21 2015 kwenye moja ya Hoteli kubwa iliyopo Sanya na kambi yao itakuwa hapo kwa muda wote mpaka siku ya fainali December 19 2015.
Kingine tunachotakiwa kukifanya ni kumpa support ya nguvu mrembo wetu Lilian Kamazima kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ambapo hiyo njia pia itamfanya asogee kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuibuka na ushindi wa Miss World 2015

Post a Comment

Previous Post Next Post