Shilingi
billion 473 zimetengwa kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu
ya juu nchini kwa mwaka huu ikilinganishwa na Shilingi bilioni 341
zilizotolewa mwaka jana ikiwa ni ongezeko la Tsh. bilioni 132 katika
bajeti ya mwaka huu.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa shirikisho la wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania(Tahliso)
bwn. Nzilanyingi John alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari
kuhusu kuaandaa mdahalo kujadili hotuba ya Rais Dkt. John Magufuli
aliyoisoma Dodoma wakati wa ufunguzi wa bunge la kumi na moja .
Alisema
kuwa kwa kipindi kifupi kumekuwa na mabadiliko ya haraka yaliyotokea
katika sekta ya elimu nchini kwa mwaka huu kwani kuna ongezeko la zaidi
ya wanafunzi 1800 waliopata mkopo ikilinganishwa na mwaka uliopita
ambapo ni wanafuzi 34128 pekee ndio waliofanikiwa kupata mkopo.
“Mpaka
sasa jumla ya wanafunzi 51,675 wa mwaka wa kwanza wamepata mkopo na
lengo ni kufikia 53,032, pia jumla ya wanafunzi 91 wa shahada ya
uzamili na wanafunzi 113 wanaosoma vyuo vya nje tayari wamepata mkopo” alisema John.
Aliongeza
kuwa katika kipindi kifupi kijacho bodi ya mikopo imehakikisha kutoa
mikopo kwa wanafunzi zaidi ya elfu moja wanaochukua Diploma maalumu ya
ualimu Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na hivyo kukamilisha adhma yao ya
kutoa mikopo kwa wanafunzi 53,032.
Aidha
shirikisho hilo ambalo ni umoja wa viongozi wa serikali za wanafunzi wa
vyuo vya elimu ya juu nchini umeandaa mdahalo wenye lengo la kutoa
fursa kwa watanzania wengi kujadili hotuba hiyo na namna rais
alivyoanza kutekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo.
Mdahalo
huo utafanyika jijini Dar es Salaam tarehe 13 mwezi huu katika ukumbi
wa Nkurumah na wazungumzaji wakuu katika mdahalo ni Mtaalamu mbobevu wa
uchumi kutoka chuo kikuu cha Mzumbe Prof.Honest Ngowi, Dkt. John Lingu
kutoka Idara ya Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na
Mwanadiplomasia Christopher Liundi.
Post a Comment