Wanawake mia wenye msukumo zaidi duniani mwaka wa 2015 wameorodheshwa na BBC.
Makala
ya mwaka huu ya Wanawake 100 ni ya tatu tangu kuanzishwa kwake 2013, na
lengo lake ni kuwakilisha wanawake vyema katika habari zinazopeperushwa
na BBC
Orodha ya mwaka huu inajumuisha mshindi wa Oscar, Mwigizaji Hillary Swank na mwanamitindo kutoka Sudan Alek Wek.
Orodha
hiyo pia inajumuisha wawekezaji 30 wenye umri wa miaka 30 kwenda chini
na wanawake wenye msukumo wa ajabu walio na miaka 80 kwenda juu.
‘Kutoogopa hatari’
Makala
haya ya BBC ya Wanawake 100 mwaka huu pia yanaangazia wahudumu wa afya
wenye ujasiri, watengenezaji filamu ambao wanabuni filamu zinazonakili
changamoto na matarajio kwenye jamii zao na pia viongozi katika nyanja
za sayansi, siasa, elimu na sanaa
Mmoja wa walioorodheshwa ni
mwakamke mmoja kutoka Argentina Estela de Carlotto 84, anayefanya kazi
ya kupatanisha watoto na wazazi wao ambao walinyakuliwa wakiwa watoto
wakati wa utawala wa kijeshi wa 1970.
Yeye mwenyewe alikutanishwa na mjukuu wake mwaka wa 2014.
Wajasiriamali wetu, ambao ni wachanga kwa vizazi viwili ukiwalinganisha na Carlotto, wanatupatia ushauri wa kuweza kufanikiwa.
Mjasiriamali
Mjerumani Antonio Albert mwenye umri wa miaka 25 ni mwanzilishi wa
Careship, ambalo huendesha huduma ya mtandaoni ya kuduma ya kuwatunza
wazee.
Anawashauri wanawake "wawe wenye ujasiri na wasiogope hatari”.
Orodha
yetu imejumuisha pembe zote za dunia kutoka kwa Li Tingting, ambaye ni
mwanaharakati wa haki za wanawake wapenzi wa jinsia moja kule Uchina
hadi kwa Chimala, Malawi, ambaye ni mkunga. Ina pia mwandishi wa vitabu
kutoka Lebanon Jana el-Hassan na mchekeshaji kutoka Marekani Megan
Grano.
Ujasiri
Baadhi ya wanawake kwenye
orodha yetu wana ujasiri sana, kwa mfano Neyda Rojas kutoka Venezuela,
mtawa ambaye hutembelea magereza nchini humo ambayo huwa yamejaa
wafungwa kupindukia. Magereza hayo ni moja ya yale hatari zaidi duniani.
Msimu huu utaanza na wiki mbili za vipindi vya kusisimua na makala mtandaoni.
Kule
India, miongoni mwa mengine tutaangazia wasichana wanaozaliwa jimbo la
mgharibi la Maharashtra, ambao hupewa jina 'nakusha' maana yake ikiwa
hawatatikani kwenye jamii. BBC itazungumza na baadhi ya wasichana
waliopewa jina hilo miaka minne iliyopita.
Tukielekea Burkina
Faso, tunakutana na wanawake walioachwa na mabwana zao waliohamia Ulaya,
baadhi kwa miezi kadha na wengine miaka.
Na kule Mashariki ya
Kati, tutazungumza na ‘Malala’ wa Syria, Maisoun Almellehan,16, ambaye
ni mkimbizi Jordan. Almellehan anajizatiti sana kuhimiza wasichana
wakimbizi waende shuleni na kusoma.
Msimu huu wa Wanawake 100
utafikia kilele kwa mjadala kuhusu sura, uongozi na mahusiano katika
maeneo 100 mbalimbali kote duniani – ikiwa ni pamoja na Albania, Kosovo,
Samoa, Fiji, Israel na Jamaica – na katika makao makuu ya BBC jijini
London.
Makala za msimu wa BBC wa Wanawake 100 zitapeperushwa
mtandaoni, katika BBC World News TV, na BBC World Service pamoja na
idhaa 28 za lugha mbalimbali kuanzia Novemba 18 hadi Desemba 2.
Post a Comment