TCRA Yavifungia Vituo 27 Vya Radio Na Tv Kwa Kukwepa Kodi.......Miongoni Mwa Vituo Vilivyofungiwa ni Star Tv, Radio Free Africa na Kiss Fm


Mamlaka ya Mawasiliano TCRA imevifungia vituo 21 vya Radio na 6 vya TV kikiwemo kituo cha Star TVRadio free AfrikaKiss Fm na Uhuru FM kwa kushindwa kulipa kodi ya lesseni kwa wakati ..
Akitangaza uamuzi huo, mkurugenzi wa habari na mawasiliano wa TCRA Innocent Mungy, amesema kuwa mitambo ya vituo hivyo itazimwa ifikapo kesho saa 6 usiku, na itawashwa baada ya vituo hivyo kulipa madeni yanayowakabili.
Mungy amesema mamlaka hiyo haiwezi kusema ni kiasi gani cha pesa ambacho vituo hivyo vinadaiwa kwa madai kuwa kanuni na taratibu haziwaruhusu kutaja kiasi hicho kwa kuwa ni siri kati ya TCRA na mteja.
Aidha Mungy amesema kuwa TCRA imewataka wadau wote wa mawasiliano nchini kutii sheria bila shuruti na kufuata taratibu, huku akisisitiza kuwa zoezi hilo la kuwasaka wanaokwepa kodi ni endelevu.
==> Vituo vingine vilivyofungiwa ni;
Sibuka FMBreez FMCountry FMEbony FMHot FMImpact FMIringa Municipal TVKiss FMKitulo FMKifimbo FMMbeya City Municipal TVRadio 5Radio Free Afrika (RFA)Musa Television NetworkPride FM radioRadio HurumaRadio UhuruStar TVRock FM RadioStandard FM radioSumbawanga Municipal TVTanga City TVTop Radio FM limitedUlanga FM 

Post a Comment

Previous Post Next Post