Mamlaka ya Mawasiliano TCRA imevifungia vituo 21 vya Radio na 6 vya TV kikiwemo kituo cha Star TV, Radio free Afrika, Kiss Fm na Uhuru FM kwa kushindwa kulipa kodi ya lesseni kwa wakati ..
Akitangaza uamuzi huo, mkurugenzi wa habari na mawasiliano
wa TCRA Innocent Mungy, amesema kuwa mitambo ya vituo hivyo itazimwa
ifikapo kesho saa 6 usiku, na itawashwa baada ya vituo hivyo kulipa
madeni yanayowakabili.
Mungy amesema mamlaka hiyo haiwezi kusema ni kiasi gani cha
pesa ambacho vituo hivyo vinadaiwa kwa madai kuwa kanuni na taratibu
haziwaruhusu kutaja kiasi hicho kwa kuwa ni siri kati ya TCRA na mteja.
Aidha Mungy amesema kuwa TCRA imewataka wadau wote wa
mawasiliano nchini kutii sheria bila shuruti na kufuata taratibu, huku
akisisitiza kuwa zoezi hilo la kuwasaka wanaokwepa kodi ni endelevu.
==> Vituo vingine vilivyofungiwa ni;
Sibuka FMBreez FMCountry FMEbony FMHot FMImpact FMIringa Municipal
TVKiss FMKitulo FMKifimbo FMMbeya City Municipal TVRadio 5Radio Free
Afrika (RFA)Musa Television NetworkPride FM radioRadio HurumaRadio
UhuruStar TVRock FM RadioStandard FM radioSumbawanga Municipal TVTanga
City TVTop Radio FM limitedUlanga FM
Post a Comment