Watu wasiyo julikana wamehack akaunti ya facebook ya msanii Belle 9 na
kuweka post yenye picha ya msanii Diamond na kuandika maneno
yanayoashiria matusi ya nguoni.
Belle99
Akizungumza na Bongo5 Alhamisi hii, Belle 9 amesema yeye anajulikana sio msanii wa kufanya vitu kama hivyo.
“Mimi sina tatizo na msanii wala sina upande wowote,” alisema Belle 9.
“Hili ni tatizo kama matatizo mengine, ni geni kwangu kwa sababu
halijawai tokea lakini kwa wasanii wengine yalishatokea. Kwa hiyo naweza
sema bado watu wangu wanaendelea kurekebisha tatizo na kuirudisha
akaunti yangu. Mimi naimani kuwa watu wameelewa kwa sio mimi kwa sababu
mimi sio mtu wa mambo hayo,” aliongeza Belle.
Post a Comment