ULAYA LEO:- MAGAZETI YANAVYOSEMA, HASA UAMISHO WA WACHEZAJI/PERUZI HAPA

NURI SAHIN AAMUA KUTUA ARSENAL, AKATAA KUPELEKWA LIVERPOOL FC

Kiungo wa Real Madrid, Nuri Sahin, mwenye umri wa miaka 23, ametaka mpango wa kupelekwa kwa mkopo Liverpool usitishwe na badala yake apelekwe Arsenal, ambayo nyota huyo wa zamani wa Dortmund anatumaini itamsaidia kung'ara kutokana na kucheza Ligi ya Mabingwa.

Fulham imefufua nia yake ya kumsajili kiungo wa Blackburn, Steven N'Zonzi, mwenye umri wa miaka 23, ambaye hayuko kwenye mipango ya Steve Kean, baada ya kugoma kuichezea klabu hiyo msimu uliopita.


Liverpool inataka kumsajli ama mmoja kati ya wachezaji wawili wa Spurs Steven Caulker au Michael Dawson, ikiwa beki Daniel Agger atahamia Manchester City.


Mshambuliaji wa Arsenal, Nicklas Bendtner amesistiza msimamo wake wa kutaka kuihama klabu hiyo, akisema kwamba hatakuwa na furaha hadi afanye hivyo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, msimu uliopita alicheza kwa mkopo Sunderland, lakini hajafanikiwa kuhamishwa moja kwa moja.


Mabingwa wa Urusi, Zenit St Petersburg wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Manchester United, Dimitar Berbatov. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 wa Bulgaria, amekwishaambiwa anaweza kuondoka Old Trafford.

Post a Comment

أحدث أقدم