MSANII WA INJILI AELEZA JINSI ALIVYONOGEWA NA MOVIE ZA NGONO a.k.a "PILAU"


Msanii maarufu wa nyimbo za injili kutoka nchini Kenya Solexx Mgenge a.k.a Gospel King amefunguka kuhusu past yake kuwa alikuwa addicted kwa kuangalia movie za ngono

Katika interview aliyofanya na mtandao wa zuqka, Solexxx alikiri kuwa alipokuwa kidato cha tano akiwa na umri wa miaka 11 kuna jirani yake aliyekuwa anasoma vidato vya juu zaidi alikuwa anaenda kwao na video cassettes za aina mbalimbali na baadhi zilikuwa ni za ngono na waliangalia wote.
 
 
Solexx alisema alinogewa sana na siku ilikuwa haipiti bila kuangalia ‘po*n*grap*ic stuff’, screen saver ya laptop yake ilikuwa na picha za wasichana wakiwa uchi, simu yake pia ilikuwa na wallpapers kibao za ngono.



King of Gospel kama anavyojiita hivi sasa, aliendelea na hali hii hadi alipofika kidato cha pili ambapo mama yake mzazi aliinasa DVD ya ngono a.k.a Pilau kwenye begi lake, na hapo akampeleka moja kwa moja kwa mtaalam wa counseling na kuanza darasa lililomsaidia kidogo, lakini ilikuwa ngumu kwa sababu washkaji zake kibao bado walikuwa wanaendelea kuangalia movie hizo na walikuwa wote mara kwa mara.

Mungu alimsaidia kuyavuka haya na ndipo akaanza kuwaza hasara kubwa aliyokuwa anaipata kwa kufatilia mikanda ya ngono, “niligundua nilikuwa natumia pesa nyingi sana kudownload po*n*g*aphic stuff, nilikuwa na zaidi ya 100GB ya moviez za ngono kwenye laptop yangu,” alifunguka.

Lakini mambo yalibadilika kabisa baada ya kuamua kuokoka na sasa anaishi maisha tofauti, sasa akiwa kama mtu aliyekwa addicted na movie hizi, huu ndio ushauri wake kwa watu wanaoangalia movie za ngono;

“Kitu ambacho wengi hawajui ni kwamba unapoteza muda mwingi sana kuangalia, na bado ni useless. Ona, unapoangalia po*n, kinachofuata ni kujaribu kitu halisi. Hiii ndo sababu  wengi wanaacha shule kwa sababu ya mimba zisizotarajiwa, na HIV/AIDS inasambazwa sana.”

Post a Comment

Previous Post Next Post