Mauaji ya Polisi wa Kenya yazidisha wito kwa Lenku, Kimaiyo kujiuzulu

Na Julius Kithuure, Nairobi

Huku Wakenya wanaposhughulika na hali ngumu ya mauaji ya watu wengi ya hivi karibuni ya maofisa polisi yaliyofanywa na majambazi katika kaunti za Turkana na Baringo, wito wa kujiuzulu kwa walio katika nafasi za uongozi za masuala ya usalama wa taifa umeongezeka.

Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Kenya David Kimaiyo na Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Taifa Joseph Ole Lenku wakiwa wamesimama kwenye kituo cha uhakiki tarehe 9 Aprili. [Tony Karumba/AFP]

Mashambulio ya kuvizia ya mwishoni mwa wiki katika kaunti ya Turkana yamefuatia baada ya wiki ya mashambulio madogo ya hapa na pale dhidi ya maofisa polisi na raia ambayo yaliua maofisa polisi wapatao 21 na raia watatu, yakiwajeruhi wengine kadhaa, na kuharibu mali za watu binafsi na polisi.

Jumamosi mchana (tarehe 1 Novemba), majambazi wenye silaha nzito walishambulia lori lililokuwa limewabeba maofisa polisi kati ya Kapedo na Lokori. Polisi hao walikuwa katika kazi maalumu ya kuchukua mabaki ya gari lililochomwa moto la Kitengo cha Huduma za Jumla (GSU) ambalo lilishambuliwa katika eneo hilo hilo wiki iliyotangulia, ambapo maofisa polisi watatu na raia watatu akiwemo mwalimu waliuawa.

Katika tukio tofauti Jumapili asubuhi sana, takribani wanaume dazani waliokuwa na silaha aina ya mapanga walijaribu kushambulia kambi ya maaskari jeshi huko Nyali, karibu na Mombasa. Askari waliokuwa katika jukumu la ulinzi walijibu mashambulizi, wakiwaua washambuliaji sita papo hapo na wa saba wakati wakikimbilia kwenye msitu ulio karibu, na mshambuliaji mmoja alikamatwa.

Askari mmoja alikatwa na panga wakati wa makabiliano, na alifariki baadaye kutokana na majeraha aliyopata katika hospitali ya Pandya huko Mombasa.

Genge lingine lenye silaha na mapanga pia lilijaribu asubuhi na mapema Jumapili kushambulia kambi ya utawala ya Malindi. Maofisa polisi walifanikiwa kuwazuia washambuliaji baada ya mapigano makali ya silaha, ingawaje washambuliaji kwanza waliharibu baadhi ya magari yaliyokuwa yameegeshwa katika kituo cha polisi.



Utokeaji wa mara kwa mara na uzito wa matukio hayo inaonyesha kwamba Inspekta Jenerali wa Polisi David Kimaiyo na Waziri wa Ndani na Uratibu wa Serikali ya Taifa Joseph Ole Lenku wamekosa udhibiti wa hali hii, baadhi ya raia wamesema, wanatoa wito wa wawili hao kujiuzulu au kuondolewa katika ofisi na Rais Uhuru Kenyatta.

Hali ya usalama 'isiyokubalika'
"Matukio haya yanaonyesha kwamba kuna kitu hakiko vizuri kuhusiana na namna Lenku na Kimaiyo wanavyoendesha chombo hichi cha usalama, na muda wa wao kutoka au kujiuzulu umewadia," alisema Robert Matano, mwenye umri wa miaka 45, mmiliki wa mgahawa wa Karibu huko Nairobi.

Matano alisema alishangaa ni maisha ya watu wangapi zaidi yatapotezwa kupotea kabla ya Kimaiyo na Lenku hawajachukua jukumu binafsi la operesheni za polisi zilizovurugwa na mikakati isiyo na ufanisi.

"Kwa hakika rais anapaswa kwa sasa kujua kwamba watu hawa wawili wanapaswa kuacha [haraka] kuongoza nafasi za juu wanazoshika," aliiambia Sabahi. "Uhuru anapaswa kuwawajibisha na kwa hilo kuwafukuza kazi kama wataendelea kung'ang'ania kukaa kwenye kazi zao."

Lenku na Kimaiyo hawajabadilisha mbinu zao za usalama licha ya mauji ya watu wengi ambayo yametokea chini ya uangalizi wao, Matano alisema.

"Tulikuwa na shambulio la kigaidi la Wesgate Septemba [2013] ambalo liliua watu wapatao 67, tarehe 15 na 16 ya mwezi Juni mashambulio huko Mpeketoni mji ulio huko Lamu ambalo liligharimu maisha ya watu 63, na sasa mauaji ya watu wengi ya maofisa polisi 21, pasipo kusahau mauji ya hapa na pale katika sehemu mblimbali nchini," alisema. "Nani atajibu kuhusu upotevu wa maisha haya na lini?"

Kiwango cha sasa cha usalama hakikubaliki, alisema mchambuzi wa masuala ya usalama mwenye makaazi huko Nairobi Mwenda Mbijiwe, akiongezea kwamba inaonekana kuwa serikali imeshindwa jukumu lake la kutoa usalama.

"Mashambulio ya ujasiri kwenye kambi ya maaskari jeshi hayakutokea kabla katika nchi hii," aliiambia Sabahi. "Ni ishara wazi ya namna hali isivyo na usalama katika taifa letu na namna uthubutu wa kufanya uhalifu ulivyo."

Maandalizi zaidi yanahitajika
Polisi wahakupaswa kuwepo katika eneo hilo pasipo kufikia matarajio katika tukio la hivi karibuni la huko Turkana kwa kuwa walipaswa kufanya upelelezi kuhusu eneo hilo na hatari zake na kuandaa mpango wa kitaalamu kushughulikia kitisho chochote kinachoweza kutokea, Mbijiwe alisema.

"Ni wazi kuwa hawakuwa wamejiandaa, ambayo kwa bahati mbaya inamanisha hawakujifunza chochote kutoka Novemba 2012 operesheni Baragoi ambayo maofisa polisi 42 walishambuliwa na kuuawa na majambazi katika kazi maalumu ya kurejesha mifugo iliyokuwa imeibiwa," alisema.

Wakati wahalifu wanaposhambulia vikosi vya usalama na kuua wengi miongoni mwao kwa tukio moja, inaonyesha hakuna aliye salama, alisema msimamizi wa zamu wa Kampuni ya Viatu ya Bata Margaret Maina, mwenye umri wa miaka 32, huko Nairobi.

"Kama polisi hawawezi kujilinda wao wenyewe, hivyo nani atatulinda sisi?" alisema, akielezea shambulio hilo kama fedheha kwa idara ya polisi.

"Kimaiyo anapaswa kuwaheshimu na kuwathamini maofisa wa ngazi za chini waliouawa wakiwa kazini kwa kukamilisha siku, ili kwamba rais awe na nafasi ya kumteua mtu mwingine mwenye uwezo wa kushawishi imani katika yombo vvya usalama," aliiambia Sabahi.

"Tumekuwa wavumilivu kwa huduma dhaifu za Lenku na Kimaiyo kwa kadiri ya muda mrefu," alisema Justus Muketha, mfanyakazi mstaafu wa benki mwenye umri wa miaka 60, akieleza kamba watu hao wawili walifanya "kuzungumza mambo mazito na kutoa tarehe za mwisho ambazo kamwe hazijawahi kufuatiwa na vitendo".

Muketha aliwakanusha watu hao kwa utaratibu wao wa "kushtukiza" katika usalama na kutoa wito wa kuacha kazi haraka "kwani mambo yamepita kiasi".

Alichukulia suala hilo pamoja na ushughulikiaji wa rais katika tukio hilo, akisema kuna ushahidi mdogo unaoonyesha hadhari ya Kenyatta ya wiki iliyopita kwamba "hatua kali" zingechukuliwa dhidi ya wale waliohusika na mashambulio imetekelezwa au washambuliaji hao wamesikiliza tahadhari yake.

Kuwajibika kwa kushindwa kwa usalama
Mwenyekiti wa Mamlaka Huru ya Kusimamia Sera (IPOA) Macharia Njeru alisema kukosekana kwa maandalizi na uratibu mzuri wa muundo wa kikosi cha polisi kwa sehemu ni kitu cha kulaumiwa kwa kutokuwepo kwa usalama.

Katika Mkutano na Vyombo vya Habari Jumatatu, Njeru alisema Kimaiyo na Mkurugenzi wa Idara ya Uchunguzi Ndegwa Muhoro wanapaswa kuwajibika kwa shambulio la maofisa polisi, kuomba radhi kwa umma na kuacha kazi badala ya kutafuta sababu.

"Kufanikiwa kwa mamlaka kumethibitisha kwamba kuwepo kwa sera zenye ufanisi kunahitaji mkakati thabiti na maandalizi ya mipango ya mwaka ikiwa ni pamoja na changamotoo za usalama na vipaumbele vinavyozingatia hali iliyopatikana katika mikoa tofauti," alisema Njeru.

Alibainisha taarifa ya hivi karibuni ya IPOA katika shambulio la Mpeketoni, akisema Kimaiyo anapaswa kutekeleza mapendekezo ya kuzuia matukio ya siku zijazo, kama vile mauaji ya Kapedo.

Julius Njuguna, mwenye umri wa miaka 44, ambaye ni msimamizi wa ulinzi wa Duka kubwa la Ridgeways huko Nairobi, alisema mashambulio ya hivi karibuni yaliacha maswali mengi yasiyokuwa na majibu na muda wa kuwauliza ni sasa.

"Kwa nini kikundi kidogo cha maofisa waliokuwa wamejiandaa bila kuwa na mpango wowote wa usaidizi walipelekwa katika kaunti ya Turkana, eneo linalofahamika kwa ujambazi, kisha siku kadhaa mapema, gari la GSU lilikuwa limetekwa na majambazi watatu na maofisa watatu waliuawa?" alisema. "Kwa nini kulikuwa hakuna kikosi cha kuwasaidia katika operesheni hiyo ya hatari?"

"Wakati maisha ya maofisa waliokuwa hawana taarifa yalipopotea katika mazingira hayo ya kizembe, maofisa wa ngazi ya juu katika usalama walipaswa kuwajibika na kuchukuliwa hatua za muhimu dhidi yao," aliiambia Sabahi.

Katika mazingira hayo ya sasa, mhitimu wa sheria katika Chuo Kikuu cha Nairobi Bernice Gathoni, mwenye umri wa miaka 39, alisema anatarajia Kimaiyo na Lenku kuachia nafasi zao.

"Kuchukua udhaifu wa mtu mwingine ni dalili ya uhodari wa kuendesha shughuli za serikali," aliiambia Sabahi. "Inaonyesha heshima kwa waliofariki, familia zao, marafiki na taifa kwa ujumla."

Wito wa utulivu, kuungwa mkono
Hata hivyo, Jonahathan Kibugi, muuzaji wa bima za maisha mwenye umri wa miaka 39 huko Nairobi alisema ilkuwa ni hali ya kutokomaa kudai viongozi wa usalama kuachia madaraka.

"Polisi wetu wameshafanya shughuli nyingi za uhalifu na ugaidi lakini ni Wakenya wachache tu waliotoa maoni kwa inspekta jenerali kwa hili," aliiambia Sabahi. "Tumpeni muda kufanya huduma ya polisi ya kisasa na kisha tutamhukumu kwa lile atakalokuwa amelikamilisha mwishoni mwa mwaka ujao."

Msemaji wa Polisi Zipporah Mboroki pia aliwaomba raia kuwa watulivu.

"Inspekta jenerali alianzisha kampeni nyingi za kuboresha operesheni za polisi na uwezo wao wa kukabiliana na tatizo," aliiambia Sabahi. "Matokeo haya hayawezi kuonekana. Anahitaji muda na kuungwa mkono na Wakenya wote ili aweze kukamilisha ahadi zake."

"Akitoa wito wa kuacha kwake kazi kila mara huduma ya taifa ya polisi inakabiliwa na changamoto ni kutokuwa na uaminifu," alisema.

Post a Comment

أحدث أقدم