
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Frasser Kashai
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Frasser Kashai, alisema ,watuhumiwa hao walikamatwa Novemba 17, mwaka huu saa 7.30 mchana katika eneo la Barabara ya 16, Kata ya Ngamiani, jijini hapa. Kamanda Kashai alisema watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa kwenye gari.
Alisema katika mahojiano na Polisi, watuhumiwa hao walikiri kuwa ni wafanyabiashara wa fedha bandia na wamekuwa wakiziuza kwa muda mrefu.
“Tulipokea taarifa kutoka kwa raia wema na ndipo tulipoanza kuwafuatilia na hatimaye kuwakamata wakiwa wamehifadhi fedha hizo ndani ya gari na katika mahojiano wamekiri kuwa wao ni wafanyabiashara wa muda mrefu,” alisema.
Alisema watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni baada ya upelelezi wa Polisi kukamilika.
CHANZO:
NIPASHE
إرسال تعليق