Mahakama ya Carolina yafungua rasmi kesi ya wanafunzi Waislamu

Baraza kuu la waamuzi limefungua mashitaka dhidi ya Craig Stephen ya mauaji ya wanafunzi watatu Waislamu.
Baraza la waamuzi wa mahakama kuu nchini Marekani jana lilimfungulia mashitaka rasmi mtuhumiwa wa mauaji ya wanafunzi watatu wa Kiislamu yaliyotokea Kaskazini mwa Carolina nchini humo.
Baraza la waamuzi wa mahakama ya jimbo la Durham lilimfungulia Craig Stephen mashitaka ya kutisha kwa kutoa silaha hadharani na ya mauaji ya Deah Barakat,23,Yusor Abu-Salha,21, na Razan Abu-Salha, 19 , kulingana na WRAL tawi la CBS.
Mauaji hayo yaliyotokea juma lililopita yalisababisha mmenyuko mkubwa katika jamii ya waislamu Marekani na kote ulimwenguni, ikiongozwa na swali kuu la kama chuki dhidi ya dini ndio iliyokuwa motisha ya mauaji hayo.
Hicks alikuwa jirani na wanafunzi hao na hapo awali, aliwahi kuhukumiwa mashitaka matatu ya shahada ya kwanza ya mauaji.
Uchunguzi wa polisi umebainisha kuwa mauaji hayo yalisababishwa na 'mzozo juu ya maegesho ya gari', lakini FBI pia imetangaza kuzindua uchunguzi tofauti kama uhalifu wa chuki.
Deah alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa pili katika Chuo Kikuu cha North Carolina kwenye kitivo cha Udaktari wa meno na Yusor ambaye alitegemea kuanza masomo yake katika shule hiyo hiyo mwaka huu, walikuwa maharusi wapya.Razan nae alikuwa ndugu yake Yusor na akisoma katika chuo hiko pia.
Familia ya waathirika wamelichukulia tukio hilo kuwa 'uhalifu wa chuki' moja kwa moja, na Baraza la Uhusiano wa Uislamu-Marekani, shirika la haki za kiraia la kiislamu, limeihusia serikali kuchunguza tukio hili bila upendeleo wa aina yoyote.
Kurasa ya Facebook kwa jina la Hicks ilibainisha chuki ya Hicks juu ya dini kutokana na alivyojitambulisha kama asiye na dini 'mpenda silaha' na maoni yake dhidi ya dini

Post a Comment

أحدث أقدم